CCM
Mlolongo wa Habari za Chama cha Mapinduzi

Kikwete amtosa Warioba
CCM Trust ni moja ya makampuni manne yanayounda kampuni ya Mwananchi Trust Limited yenye hisa katika kampuni ya Mwananchi Gold Limited (MGL) ya Dar es Salaam.

Sisiem wamenasa penyewe
KATIKA miaka ya 1980 lilikuwepo basi lililobatizwa jina la Navalonge Swela, ambalo lilikuwa linafanya safari zake kati ya Njombe na Dar es Salaam.

CCM yaanza kuaga ikulu
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeanza kufanya maandalizi ya kuaga ikulu na kuwa kiongozi mkuu wa upinzani bungeni, MwanaHALISI limeelezwa.

CCM waanza kugombania mbao
HATA kabla mashua yao haijapasuka kabisa, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaonekana kuanza kugombania mbao za mashua yao hiyo.
Kauli mchanganyiko zilizotolewa na baadhi ya viongozi wa CCM hivi karibuni zinaacha mashaka makubwa kwa mustakabari wa chama hicho.
Wengi wa viongozi hao wamekatishwa tamaa na uongozi wa chama chao kilichokosa nguvu ya Mwenyekiti.
CCM walidakia mradi wa CHADEMA wa vita dhidi ya ufisadi, ukawashinda. Walipogundua kosa, wakaanzisha wa kwao wakaupachika jina kujivua gamba ambao sasa umewatumbukia nyongo.

CCM wakiri gamba limekwama
KWA mwaka mzima uliopita Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kinaimba na kurudia kibwagizo cha wimbo wa kuvuana magamba.

CCM inanengua midundo ya CHADEMA
NAFURAHISHWA na siasa za Tanzania sasa kwa maana moja kubwa, kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM), mbali ya kujigamba kuwa hakuna kiongozi wa chama vya upinzani ambaye hakutokana nacho, kwa vitendo, kimethibitisha kuwa sasa kinafundishwa siasa na vyama vya upinzani.

CCM ‘imejiua’, inasubiri kuzikwa
POLISI wa kitengo cha barabarani (trafiki) anapopata taarifa ya ajali, kitendo cha kwanza huwa ni kwenda kwenye eneo la tukio. Akifika atapima ilipotokea ajali ili kubaini chanzo na mkosaji.

CCM kweli wanachonga vinyago
AKIHUTUBIA mkutano wa hadhara, alipokuwa katika mji mdogo wa Makambako mkoani Njombe, Katibu wa Uenezi na Itikadi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye aliuliza wananchi, “Nani yuko upinzani ambaye hakutoka CCM?”

Rushwa bungeni ni zaidi ya uhaini
TAARIFA za Bunge au wabunge kujihusisha na vitendo vya rushwa ni za hatari sana. Kwanza, hata kuzusha tu kuwa wabunge wanapokea rushwa ni hatari isiyovumilika kwa sababu watu wengi wamezoea kuona wabunge wanahonga si kuhongwa.

CCM, CUF jino kwa jino
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) vimeanza kufarakana; na serikali yao ya pamoja inaweza kusambaratika wakati wowote, MwanaHALISI limeelezwa.

CCM imevuruga vita dhidi ya ufisadi
MATUKIO mawili makubwa yalifanyika hivi karibuni. Jijini Dar es Salaam Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilifanya mkutano wa hadhara katika viwanja vya Jangwani, huku Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikifanya mikutano ya ndani wilayani Misenyi mkoa wa Kagera.

Sisiem inasubiri maombi
MTU akiugua, hujikokota hadi hospitalini kutafuta tiba. Ikiwa amezidiwa, ndugu na jamaa ndio humchukua na kumpeleka. Huko ugonjwa hushitakiwa na kuadhibiwa na madaktari kwa njia ya vidonge au sindano.

JK: Ruksa Lowassa kuhama
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amewataka wanachama wote wa chama hicho wanaoona hakikaliki, kuhama badala ya kubaki wakilalamika.

Acha ufisadi uiue CCM
SASA zipo kila dalili kwamba ufisadi ndio sababu kuu itakayochangia kuanguka kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Ufisadi umedhoofisha mifumo yote ya uongozi katika chama chenyewe na tayari umehamia kisawasawa kwenye serikali inayoiongoza.
Tunaona hata pale serikali inapopeleka bungeni sheria mpya kwa nia ya kutatua tatizo fulani, ufisadi unapenya na kuiviza isitekelezeke.
Ndio maana zipo sheria nyingi zikiwemo nzuri tu, lakini bado hazijaleta ufumbuzi wa matatizo mbalimbali yanayokera jamii.

Ni nani aliye msafi ndani ya CCM
SASA hakuna anayeshangaa katika nchi hii anapopita mitaani, vijijini, machimboni na makondeni na kusikia watu wanasema kuwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakuna aliyemsafi.
Ni jambo la kawaida hata ndani ya CCM wenyewe hawashangazwi na kauli hii. Mara nyingi ukweli haushangazi.
CCM wenyewe hawajishangai kwa sababu wanawaza namna moja. Watu wa fani moja huwa hawajishangai wakiwa katika fani yao mpaka pale wanapojilinganisha au kujitofautisha na watu wa fani nyingine au wasio na fani.

CCM inanufaika na umaskini wetu
SIKUSHANGAA kusikia habari zilizoandikwa kwenye magazeti wiki iliyopita zikieleza kuwa mtu mmoja kajinyonga kwa kutumia fulana ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Huu ni ushahidi kuwa mtu huyo ni maskini kiasi kwamba hana uwezo wa kununua kamba ya katani ya kujinyongea.
Yaelekea bwana yule aliyejinyonga, hana shuka na kwamba usiku yeye hulala bila kuvua hiyo fulana ya njano ya CCM aliyohongwa wakati wa uchaguzi mkuu wa 2010.
Bwana huyo angekuwa na shuka angeitumia kujinyonga kwani shuka, kanga na kitenge vinafaa kujinyongea kuliko fulana.

CCM, CHADEMA wanacheza zero distance
KUNA vita ya kugombania nchi ambayo inaendelea. Labda niseme vizuri zaidi kuwa kuna mpambano unaendelea wa kugombania nani atawale nchini; na katika hili hakuna urafiki, udugu, mapatano au umoja wa ulaghai.

CCM sasa wamevuna walichopanda
JOSHUA Nasari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameibuka kidedea katika kinyang’anyiro cha ubunge Arumeru Mashariki.

CCM inaongoza nchi kwa chuki
MATUKIO yanayoonyesha kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaongoza nchi hii kwa chuki ni mengi na yanathibitika.

CCM wana ugonjwa wa kusahau
KATIKA maisha yake yote, Bogi Benda alikuwa msumbufu. Mtu wa vituko, dharau, kejeli. Bali alivumiliwa kwa vile alikuwa ‘bosi’.
Kuna wakati alipotaka kuzima hoja fulani ili kusumbua tu watu, aliamua kulala na kukoroma kwenye vikao.
Kuna siku alikwenda hospitali akitaka atibiwe ugonjwa wa kusahau aliodai unamsumbua sana. Akabahatika. Alimkuta daktari nje na hapohapo akamweleza kinachomsumbua.

CCM ina uchawi mkali, umma umelogwa
NIMEJIPA fursa ya kufuatilia kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Arumeru Mashariki zilizopamba moto kwa wiki ya pili sasa.

CCM inaringia kikombe cha mateso
UKITAKA kujua raha wanayopata wafuasi wa chama tawala, tazama tabu wanayopata wanachama wa kambi ya upinzani – kupigwa, kujeruhiwa na kuuawa.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetengeneza kikombe hicho cha mateso kwa miaka 20 na inahaha kuhakikisha hakishikwi na upinzani.
Hata Mungu alipowaambia wana wa Israel waondoke Misri, ni Mungu huyo huyo aliyewapa Mafarao wa Misri moyo mgumu. Siku ya mwisho ilipofika Mafarao walipata pigo, jeshi lao liliangamia baharini huku Waisrael wakienda zao.

Miaka 20 ya mapandikizi ya CCM
MAGEUZI yalipoanza na hatimaye mfumo wa vyama vingi kuruhusiwa rasmi nchini mwaka 1992, watu waliotamani kuwa viongozi lakini wakawa wanakosa nafasi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) walijiunga na vyama vya upinzani.

CCM mnasikitisha
MWENENDO wa uongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unasikitisha mno. Masikitiko yenyewe ni yale yanayotokana na utamaduni mbaya wa kuujua ukweli, halafu kwa makusudi, viongozi wakaamua kuudharau.

CCM na Tanzania tuitakayo
SIFA moja kubwa kwa serikali hii inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni kuacha aibu ipite bila kutolea majibu.
Nchi imeshuhudia hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete akitofautiana na kumkana Waziri mkuu, Mizengo Pinda pamoja na Spika wa Bunge la Jamhuri, Anne Makinda. Haya yamefanyika hadharani.
Ongezeko la posho za wabunge ndilo lilisababisha ofisi hizo tatu kujiumauma na kutofautiana wazi. Spika na Waziri mkuu walidai posho hizo ni halali, lakini ikulu baada ya kusoma kasi ya upepo wa upinzani ikasema ni haramu.

Kifo ndiyo tiba pekee kwa CCM
WIKI iliyopita nilihitimisha makala yangu kwa kugusia kidogo juu ya sherehe za miaka 35 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kufeli huku ni kushindwa sera za CCM
KARIBU nusu ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kumaliza kidato cha nne mwaka jana wamefeli. Matokeo yameonyesha kuwa ni asilimia 53.59 tu ya wanafunzi waliofanya mtihani wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) ndio waliofaulu katika viwango mbalimbali.
Takwimu hizo pia zinaonyesha jambo jingine: Kati ya wale waliofaulu wavulana ni wengi zaidi kuliko wasichana.
Je, kufeli huku kuna maana gani? Jibu liko wazi: Sera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuhusu elimu pamoja na kutumia mamilioni ya shilingi, imeshindwa.

CCM wamekanyaga sheshere
SERIKALI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaelekea imekanyaga mdudu mchafuzi. Mdudu huyo Zanzibar anaitwa sheshere, Wabena humwita hilufi, Wasangu wanamwita shilufyana Wahaya humwita …
Mtu akikanyaga sheshere, hawezi kufika anakokwenda; atazunguka sana, atapitiliza hata eneo analokwenda hadi ashikwe au asimamishwe na mtu anayemfahamu.

CCM wajiaibisha
KWA kile kilichoonyeshwa hadharani kama onyesho maalum la Sungusungu, mara tu ugawaji wa kadi kwa wanachama wapya ulipokoma, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimechoka.

CCM isiporejea asili itajuta -Nkumba
MBUNGE wa Sikonge, Saidi Juma Nkumba ni mmoja wa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaokiri chama chao kimepoteza asili yake.
Nkumba, aliyeingia bungeni kipindi cha tatu mfululizo mwaka 2010, anasema, “CCM lazima irejee kwenye misingi yake ya asili.”
Anaitaja misingi hiyo kuwa ni kutetea wanyonge ambao amesema kuwa kwa muda mrefu sasa wamekuwa wakilalamika kuachwa solemba.