Chenge
Mlolongo wa Habari zinazomhusu Andrew Chenge
Kikwete atavua magamba mangapi?
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), sasa kinatafuta mlango wa kutokea baada ya kushindwa kutekeleza kwa vitendo mradi wake wa kujivua gamba.
Ukweli wa kama kimeshindwa kujivua gamba uko wazi, kinachokosekana sasa ni ujasiri wa kukiri hadharani kuwa kimeshindwa.
Tangu kushindwa kutekeleza mradi huo, kumekuwa na kauli tofauti zinazotafuta kupunguza makali ya aibu ya kushindwa kutoka kwa viongozi wakuu wa chama hicho.
Kwa mfano, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wiki iliyopita, Wilson Mukama, katibu mkuu wa chama hicho, amenukuliwa akisema, “Sharti

Gamba lamponza Kikwete
MRADI wa kujivua gamba umeanza kumyumbisha Rais Jakaya Kikwete. Baadhi ya marafiki zake tayari wamegawanyika; wengine wameanza kukata tamaa na wengine wanajisalimisha kwa wanaotuhumiwa ufisadi, MwanaHALISI linaweza kuripoti.

Kikwete maji ya shingo
RAIS Jakaya Kikwete amebakiwa na njia mbili tu kulinda nafasi yake katika Chama cha Mapinduzi (CCM).

Kikwete kigeugeu
- Anauma na kupuliza
- ‘Auchuna’ kuhusu ufisadi
RAIS Jakaya Kikwete sasa ana sura mbili. Akiwa serikalini anauma. Akiwa kwenye chama chake anapuliza.

Nape amgeukia Kikwete
NAPE Nnauye, katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) amemjia juu Rais Jakaya Jakaya Kikwete na kusema, “ni sehemu ya chimbuko la migawanyiko inayokikumba chama chake,” imeelezwa.
Serikali yasubiri kuanguka
ALICHOKIFANYA Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe bungeni mnamo wiki iliyopita, juu ya tuhuma za rada zinazomkabili Andrew Chenge ni udhalilishaji dhidi ya serikali na wananchi.

Chenge, Chikawe sasa wamjaribu Rais Kikwete
MRADI wa “kumtakasa” aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali (1995-2006), Andrew Chenge, kwa mara nyingine, umeshindwa. Pamoja na jitihada kubwa za washirika wa Chenge katika mradi huo, bado utakaso haujaweza kutimia.

Watumishi wanaugua posho, uvivu
TUJIULIZE maswali magumu leo. Hivi kama akina Edward Lowassa, Andrew Chenge na Rostam Aziz wakijivua nyadhifa zao zote ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakaachia ubunge wanaoshikilia kule Monduli, Bariadi Magharibi na Igunga, tutakuwa tumetatua matatizo ya kuzorota kwa utumishi wa umma?

Watuhumiwa aina ya Chenge wametuloga
WAAFRIKA wana kitu kimoja kinachowaunganisha, pale wanapokosa jibu katika mambo magumu yanayokabili na kuhitaji kusumbua bongo, jibu lao huwa rahisi mno – kulogwa.

Lowassa amkatia rufaa Kikwete
- Atinga kwa Nabii Joshua kuombewa
- Waziri Membe ateta na Rostam Aziz
EDWARD Lowassa, mwanasiasa anayetajwa “kujipanga kugombea urais mwaka 2015,” ametinga nchini Nigeria kufanya maombi, MwanaHALISI limeelezwa.

Lowassa, Rostam kumzima Kikwete
- Waahidi kumlipua vikaoni
- CCM hatihati kuvunjika
HATUA yoyote ya Rais Jakaya Kikwete kutaka kuwafukuza ndani ya Chama Chaa Mapinduzi (CCM) wanaowaita “watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini,” yaweza kumuumiza mwenyewe, MwanaHALISI limeelezwa.

Mafisadi ‘kaa la moto’
RAIS Jakaya Kikwete ameonyesha kutokuwa na uwezo wa kufukuza wenzake ambao wametuhumiwa ufisadi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

CCM yafyata kwa mafisadi
VIONGOZI wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameshindwa kuwaondoa katika chama hicho wale wanaowaita watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, imefahamika.

Lowassa, Rostam, Chenge bado
PAMOJA na tambo za viongozi wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutaka kuwafukuza ndani ya chama hicho watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge, bado kimeshindwa kuwapa barua za kuwafukuza.

JK ameshindwa kunusuru chama chake
RAIS Jakaya Kikwete ameshindwa kukiokoa chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka katika tope la ufisadi. Kile alichoita, “CCM kujivua gamba, kimeishia kuchuna ngozi.”

Chenge ‘wa vijisenti’ bado hajasafishwa
ANDREW Chenge, yule mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali (1995-2006), bado hajatakasika kutokana na lundo la tuhuma za ununuzi wa rada kwa “bei ya kuruka” kutoka Uingereza.

Chenge ataka kuunajisi uspika
TANZANIA ingekuwa ni nchi inayojali japo kwa chembe tu uadilifu, mtu kama Andrew Chenge hasingethubutu kuwania nafasi yoyote ya kuchaguliwa na wananchi. Kikubwa ambacho angelikifanya ni kuendesha biashara zake.
‘Vyama vya msimu’ vyatibua ushindi wa kishindo wa CCM
MARA nyingi washindi huwa wanatamba; “Uwe halali, wa mizengwe au wa kupora ushindi ni ushindi.” Haya ni maneno ya kishabiki maarufu kwa mashabiki wa mpira ambao baada ya mechi watazungumzia kwenye vijiwe vyao namna ushindi ulivyopatikana.

Chenge, Mramba, Karamagi na Rostam wasirudi bungeni
KWANZA, ni lazima ifahamike kwamba tunapotaka kujenga demokrasia katika taifa, msingi mmoja mkuu ni viongozi kufahamu kuwa uongozi ni utumishi.
Katika msingi huo tulirudia mara kwa mara mawazo kuwa “cheo ni dhamana.” Mawazo haya yote yalitaka kutuonesha kwamba anayetaka kuwa kiongozi wa umma ni lazima atambue kuwa anataka kuwa mtumishi wa umma.
Katika utumishi huu wa umma jambo kubwa zaidi ni imani ya wananchi kwa viongozi wao. Endapo wananchi wanaanza kupoteza imani na viongozi wao, basi viongozi hao wanakuwa hawana mahali tena pa kusimamia.

Ukitaka meza wembe, Chenge haguswi
“SAFARI hii tumekuwa makini sana katika kufikia mkataba na Rites kuendesha TRL,” hii ilikuwa ni sehemu tu ya kauli ya aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge.

Serikali kufanya usanii rada
- Yaweza kuwatema akina Chenge
- Waokotwa ‘vijana wa Kariakoo’
KESI ya "vigogo wa rada" imehamia kwa watu wadogo ikiacha watuhumiwa wakuu wa awali – Andrew Chenge, Tanil Sumaiya na Sailesh Vithal, imefahamika.

Rada kumuumbua Mkapa
- Lipumba ataka Bunge lichunguze
- Hata dili za helikopta na ndege ya rais
BAADA ya kampuni iliyouza rada kwa serikali kukiri kutumia rushwa, Bunge limeombwa kuchunguza mikataba yote mikubwa inayomuhusisha mfanyabiashara Sailesh Vithlan.

RADA imewafunua watawala, watajificha wapi?
KUNA kitu kinaitwa bahati. Wapo watu waliozaliwa na bahati, mafanikio yao katika maisha hayafanani hata chembe na bidii wanayotia katika kujitafutia maisha.

Nyumba ya Kikwete inaungua
KAMATI ya rais mstaafu Ali Hassani Mwinyi iliyoundwa kutafuta "kiini cha uhasama" miongoni mwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), imezidisha nyongo.

Chenge: Jasiri asiyeacha asili
JASIRI haachi asili! Ni Andrew Chenge. Wiki iliyopita, bila kutafuna maneno Chenge alithibitisha kuwa bado ni shujaa wa mikataba.

Naona Chenge akimfuata Mramba, Yona
DUNIA ina mambo. Kuna siku moja rafiki yangu wa karibu sana alinisimulia kisa cha kuchekesha na kushangaza. Hiki hakikuwa kingine isipokuwa kilihusu ugomvi wa mwanasiasa maarufu nchini, Andrew Chenge na mwandishi wa habari mwandamizi, jina ninahifadhi, kilichotokea katika klabu moja jijini Dar es Salaam miaka ya hivi karibuni.

Nani atafuata nyayo za Pinda?
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Mizengo Pinda, amejiandikia historia kwa kufanya mambo mawili makubwa.

Watuhumiwa wa ufisadi hawasafishiki
WALE wanaoitwa watuhumiwa wa ufisadi hawajasafishwa. Vikao vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) vilivyofanyika mkoani Dodoma wiki mbili zilizopita, kamwe haviwezi kuwasafisha.

Chenge na tuhuma mpya
- Ni ushirikina ukumbi wa Bunge
ANDREW Chenge, ambaye anakabiliwa na tuhuma za "ufisadi" sasa ametoswa katika tuhuma mpya za ushirikina.

Taifa la JK linajiendea lenyewe
Lazima tukubaliane kwamba taifa hili kwa sasa halina viongozi wa kutoa mwelekeo, lawama zote zikiendee Chama Cha Mapinduzi (CCM) Chama tawala.