Lowassa
Mlolongo wa Habari zinazomhusu Edward Lowassa

Lowassa kuibukia bungeni
- 'Majemedari' wake wajipanga
- Kikwete huenda akahusishwa
EDWARD Lowassa, aliyekuwa waziri mkuu, anatarajiwa kuibukia katika mkutano ujao wa Bunge na kupasua kile kinachoitwa "ukweli kuhusu utata wa mkataba wa Richmond," imefahamika.

Lowassa, Msabaha hapatoshi
- Ni katika sakata la Richmond
- Kila mmoja apanga kujinasua
HATMA ya Edward Lowassa kujinasua kwenye kashfa ya mkataba tata wa kampuni ya Richmond, ipo mikononi mwa Dk. Ibrahim Msabaha, MwanaHALISI limeelezwa.
Mbio za urais zaingia kanisani
- Lowassa tayari ashika mwaliko wa 2013
- Sitta, Membe wapigana vikumbio
- Mbowe: Mimi hasitaki urais
MAKADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kutaka urais mwaka 2015, wameanza mbio katika nyumba za ibada, MwanaHALISI imebaini.

Lowassa anajua uzalendo au ni ‘machozi ya mamba?’
EDWARD Lowassa, yule aliyejiuzulu nafasi ya waziri mkuu kutokana na kashifa ya kuingiza nchi kwenye mkataba wa kinyonyaji wa makampuni ya Richmond/Dowans, sasa anasaka utakaso.
Kikwete atavua magamba mangapi?
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), sasa kinatafuta mlango wa kutokea baada ya kushindwa kutekeleza kwa vitendo mradi wake wa kujivua gamba.
Ukweli wa kama kimeshindwa kujivua gamba uko wazi, kinachokosekana sasa ni ujasiri wa kukiri hadharani kuwa kimeshindwa.
Tangu kushindwa kutekeleza mradi huo, kumekuwa na kauli tofauti zinazotafuta kupunguza makali ya aibu ya kushindwa kutoka kwa viongozi wakuu wa chama hicho.
Kwa mfano, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wiki iliyopita, Wilson Mukama, katibu mkuu wa chama hicho, amenukuliwa akisema, “Sharti

Kikwete, Lowassa hapatoshi
HATIMAYE Edward Lowassa ametoka hadharani na kuonyesha kuwa anataka kupimana ubavu na Rais Jakaya Kikwete.
Kikwete mtuhumiwa, tufanye nini?
UKURASA mpya kuhusu sakata la Richmond, umefunguliwa baada ya mambo mawili kutokea katika vikao vya Chama Cha Mapinduzi (CCM), vilivyomalizika mjini Dodoma Alhamisi iliyopita.

Mjadala wa Richmond urejeshwe tena bungeni
RIPOTI ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba tata kati ya serikali na kampuni ya kufua umeme wa dharula ya Richmond Development Company (RDC), hatimaye “imekamilika.”
Lowassa: Hii ni furaha ya muda
VIKAO vikuu vya maamuzi vya Chama cha Mapinduzi (CCM) – Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) vilivyofanyika wiki iliyopita, vimekubaliana kulirejesha suala zima la kuleta mageuzi ya kisiasa ndani ya chama hicho, maarufu kwa msemo wa kujivua gamba, katika kamati za usalama na maadili za ngazi ya tawi hadi taifa.
Huo umeelezwa ni uamuzi unaolenga kuchukua hatua dhidi ya wote waliohusika kukishushia hadhi chama hicho mbele ya jamii, kwa kujihusisha na mambo yanayokwenda kinyume na maadili ya uongozi, vikiwamo vitendo vya ufisadi, kwa kufuata taratibu na kanuni zilizowekwa na c

Namhurumia rais wangu Kikwete
WIKI iliyopita ilikuwa mbaya sana kwa rais wangu, Jakaya Mrisho Kikwete, kwa namna alivyoumbuliwa mkutanoni na rafiki yake, Luteni wa Jeshi Mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa, ambaye tumeambiwa mara nyingi kuwa hawakukutana barabarani.
Katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika Dodoma , Lowassa alipewa dakika saba tu kusema jambo naye akazitumia vilivyo, kwa kifupi na kwa ufasaha.
Nimeambiwa na wale waliokuwapo Dodoma , ndugu zangu wa Mwananchi, kama walivyoripoti katika gazeti lao, kwamba Lowassa alisema:
“Mwenyekit

Ikulu aibu tupu
VIGOGO kadhaa waandamizi serikalini na katika bunge wamenufaika na mamilioni ya shilingi yaliyokusanywa kinyume cha taratibu na David Jairo, katibu mkuu wizara ya nishati na madini, MwanaHALISI limeelezwa.

Gamba lamponza Kikwete
MRADI wa kujivua gamba umeanza kumyumbisha Rais Jakaya Kikwete. Baadhi ya marafiki zake tayari wamegawanyika; wengine wameanza kukata tamaa na wengine wanajisalimisha kwa wanaotuhumiwa ufisadi, MwanaHALISI linaweza kuripoti.
Edward Lowassa: Usifanye kosa la pili
MACHO na masikio ya Watanzania yako Dodoma kudodosa nini kitatokea huko, kunakofanyika vikao vya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kwa kuwa hiki ndicho chama tawala na Watanzania kama watawaliwa, wana haki ya kujua nini kinaamuliwa na chama tawala.
Zimwi la Richmond bado lamuandama Lowassa
VIONGOZI waliokuwa serikalini wakati wa mkataba wa kuzalisha umeme wa dharula wa Richmond bado wanaendelea kung’ang’aniwa kwenye kashifa ya kushiriki kwenye ufisadi wa mkataba huo, MwanaHALISI limeelezwa.

Kikwete maji ya shingo
RAIS Jakaya Kikwete amebakiwa na njia mbili tu kulinda nafasi yake katika Chama cha Mapinduzi (CCM).

Siri za Nape nje
- Ni zile zinazomhusu Lowassa
- Profesa Mwandosya pia atajwa
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya taifa (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amejiingiza katika mradi wa kutafuta mrithi wa Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, imefahamika.

Nape amgeukia Kikwete
NAPE Nnauye, katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) amemjia juu Rais Jakaya Jakaya Kikwete na kusema, “ni sehemu ya chimbuko la migawanyiko inayokikumba chama chake,” imeelezwa.

Kikwete hajamjibu Lowassa
RAIS Jakaya Kikwete, ama ameshindwa au amekataa kujibu tuhuma za swahiba wake, kwamba serikali yake inaumwa ugonjwa wa kutofanya maamuzi magumu, MwanaHALISI limeelezwa.

Mwisho wa maswahiba CCM
IPO mifano mingi ya kuonyesha namna viongozi marafiki wasivyoweza kutawala pamoja. Watapingana hadharani, watakorofishana na mwisho, mmoja hutafuta mbinu za kumpoteza mwingine kisiasa.

Watumishi wanaugua posho, uvivu
TUJIULIZE maswali magumu leo. Hivi kama akina Edward Lowassa, Andrew Chenge na Rostam Aziz wakijivua nyadhifa zao zote ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakaachia ubunge wanaoshikilia kule Monduli, Bariadi Magharibi na Igunga, tutakuwa tumetatua matatizo ya kuzorota kwa utumishi wa umma?
Ni uamuzi mgumu, utapeli au ajali ya kisiasa?
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amelidanganya tena Bunge. Amedai serikali ya awamu ya nne imefanya maamuzi mengi magumu kuliko serikali nyingine yoyote iliyotangulia. Hii ni kejeri ya aina yake na ninaamini rais mstaafu Benjamin Mkapa alipomsikia Pinda akitoa kauli hiyo alishikwa na bumbuwazi.

Lowassa amchokoza Kikwete
EDWARD Lowassa, waziri mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, “amemtia kidole jichoni” Rais Jakaya Kikwete.

CCM watoana roho kwa urais
RAIS Jakaya Kikwete ameendelea kukaa kimya huku viongozi wake wakianza “kutoana roho” kwa urais wa 2015, MwanaHALISI limeelezwa.

Lowassa amkatia rufaa Kikwete
- Atinga kwa Nabii Joshua kuombewa
- Waziri Membe ateta na Rostam Aziz
EDWARD Lowassa, mwanasiasa anayetajwa “kujipanga kugombea urais mwaka 2015,” ametinga nchini Nigeria kufanya maombi, MwanaHALISI limeelezwa.

Lowassa, Rostam kumzima Kikwete
- Waahidi kumlipua vikaoni
- CCM hatihati kuvunjika
HATUA yoyote ya Rais Jakaya Kikwete kutaka kuwafukuza ndani ya Chama Chaa Mapinduzi (CCM) wanaowaita “watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini,” yaweza kumuumiza mwenyewe, MwanaHALISI limeelezwa.

Mafisadi CCM wageuka mbogo
- Lowassa, Rostam wamkoromea Msekwa
SASA ni piga ni kupige ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wanakataa kujiuzulu, MwanaHALISI limeelezwa.
Ni ubaya wa Lowassa au udhaifu wa JK?
KADRI siku zinavyosonga mbele, hali ya baadaye ya chama chetu – Chama Cha Mapinduzi (CCM) – ndivyo inavyozidi kutatanisha. Wanachama na wapenzi wa chama wamechanganyikiwa kwa sababu hawana kiongozi wanayeweza kumwamini ili awaelekeze waelekee wapi.

Mafisadi ‘kaa la moto’
RAIS Jakaya Kikwete ameonyesha kutokuwa na uwezo wa kufukuza wenzake ambao wametuhumiwa ufisadi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

CCM yafyata kwa mafisadi
VIONGOZI wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameshindwa kuwaondoa katika chama hicho wale wanaowaita watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, imefahamika.

Lowassa, Rostam, Chenge bado
PAMOJA na tambo za viongozi wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutaka kuwafukuza ndani ya chama hicho watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge, bado kimeshindwa kuwapa barua za kuwafukuza.