Lowassa


Mlolongo wa Habari zinazomhusu Edward Lowassa

Saed Kubenea's picture

Lowassa kuibukia bungeni


Na Saed Kubenea - Imechapwa 01 November 2009

'Majemedari' wake wajipanga
Kikwete huenda akahusishwa

EDWARD Lowassa, aliyekuwa waziri mkuu, anatarajiwa kuibukia katika mkutano ujao wa Bunge na kupasua kile kinachoitwa "ukweli kuhusu utata wa mkataba wa Richmond," imefahamika.

Saed Kubenea's picture

Lowassa, Msabaha hapatoshi


Na Saed Kubenea - Imechapwa 28 October 2009

Ni katika sakata la Richmond
Kila mmoja apanga kujinasua

HATMA ya Edward Lowassa kujinasua kwenye kashfa ya mkataba tata wa kampuni ya Richmond, ipo mikononi mwa Dk. Ibrahim Msabaha, MwanaHALISI limeelezwa.

Jacob Daffi's picture

Mbio za urais zaingia kanisani


Na Jacob Daffi - Imechapwa 18 January 2012

Lowassa tayari ashika mwaliko wa 2013
Sitta, Membe wapigana vikumbio
Mbowe: Mimi hasitaki urais

MAKADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kutaka urais mwaka 2015, wameanza mbio katika nyumba za ibada,  MwanaHALISI imebaini.

Saed Kubenea's picture

Lowassa anajua uzalendo au ni ‘machozi ya mamba?’


Na Saed Kubenea - Imechapwa 18 January 2012

EDWARD Lowassa, yule aliyejiuzulu nafasi ya waziri mkuu kutokana na kashifa ya kuingiza nchi kwenye mkataba wa kinyonyaji wa makampuni ya Richmond/Dowans, sasa anasaka utakaso.

Jacob Daffi's picture

Kikwete atavua magamba mangapi?


Na Jacob Daffi - Imechapwa 07 December 2011

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), sasa kinatafuta mlango wa kutokea baada ya kushindwa kutekeleza kwa vitendo mradi wake wa kujivua gamba.

Ukweli wa kama kimeshindwa kujivua gamba uko wazi, kinachokosekana sasa ni ujasiri wa kukiri hadharani kuwa kimeshindwa.

Tangu kushindwa kutekeleza mradi huo, kumekuwa na kauli tofauti zinazotafuta kupunguza makali ya aibu ya kushindwa kutoka kwa viongozi wakuu wa chama hicho.

Kwa mfano, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wiki iliyopita, Wilson Mukama, katibu mkuu wa chama hicho, amenukuliwa akisema, “Sharti

Saed Kubenea's picture

Kikwete, Lowassa hapatoshi


Na Saed Kubenea - Imechapwa 30 November 2011

HATIMAYE Edward Lowassa ametoka hadharani na kuonyesha kuwa anataka kupimana ubavu na Rais Jakaya Kikwete.

Kondo Tutindaga's picture

Kikwete mtuhumiwa, tufanye nini?


Na Kondo Tutindaga - Imechapwa 30 November 2011

UKURASA mpya kuhusu sakata la Richmond, umefunguliwa baada ya mambo mawili kutokea katika vikao vya Chama Cha Mapinduzi (CCM), vilivyomalizika mjini Dodoma Alhamisi iliyopita.

Saed Kubenea's picture

Mjadala wa Richmond urejeshwe tena bungeni


Na Saed Kubenea - Imechapwa 30 November 2011

RIPOTI ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba tata kati ya serikali na kampuni ya kufua umeme wa dharula ya Richmond Development Company (RDC), hatimaye “imekamilika.”

Mayage S. Mayage's picture

Lowassa: Hii ni furaha ya muda


Na Mayage S. Mayage - Imechapwa 30 November 2011

VIKAO vikuu vya maamuzi vya Chama cha Mapinduzi (CCM) – Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) vilivyofanyika wiki iliyopita, vimekubaliana kulirejesha suala zima la kuleta mageuzi ya kisiasa ndani ya chama hicho, maarufu kwa msemo wa kujivua gamba, katika kamati za usalama na maadili za ngazi ya tawi hadi taifa.

Huo umeelezwa ni uamuzi unaolenga kuchukua hatua dhidi ya wote waliohusika kukishushia hadhi chama hicho mbele ya jamii, kwa kujihusisha na mambo yanayokwenda kinyume na maadili ya uongozi, vikiwamo vitendo vya ufisadi, kwa kufuata taratibu na kanuni zilizowekwa na c

Nyaronyo Kicheere's picture

Namhurumia rais wangu Kikwete


Na Nyaronyo Kicheere - Imechapwa 30 November 2011

WIKI iliyopita ilikuwa mbaya sana kwa rais wangu, Jakaya Mrisho Kikwete, kwa namna alivyoumbuliwa mkutanoni na rafiki yake, Luteni wa Jeshi Mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa, ambaye tumeambiwa mara nyingi kuwa hawakukutana barabarani.

Katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika Dodoma , Lowassa alipewa dakika saba tu kusema jambo naye akazitumia vilivyo, kwa kifupi na kwa ufasaha.

Nimeambiwa na wale waliokuwapo Dodoma , ndugu zangu wa Mwananchi, kama walivyoripoti katika gazeti lao, kwamba Lowassa alisema:

“Mwenyekit

Saed Kubenea's picture

Ikulu aibu tupu


Na Saed Kubenea - Imechapwa 23 November 2011

VIGOGO kadhaa waandamizi serikalini na katika bunge wamenufaika na mamilioni ya shilingi yaliyokusanywa kinyume cha taratibu na David Jairo, katibu mkuu wizara ya nishati na madini, MwanaHALISI limeelezwa.

Mwandishi wetu's picture

Gamba lamponza Kikwete


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 23 November 2011

MRADI wa kujivua gamba umeanza kumyumbisha Rais Jakaya Kikwete. Baadhi ya marafiki zake tayari wamegawanyika; wengine wameanza kukata tamaa na wengine wanajisalimisha kwa wanaotuhumiwa ufisadi, MwanaHALISI linaweza kuripoti.

Kondo Tutindaga's picture

Edward Lowassa: Usifanye kosa la pili


Na Kondo Tutindaga - Imechapwa 23 November 2011

MACHO na masikio ya Watanzania yako Dodoma kudodosa nini kitatokea huko, kunakofanyika vikao vya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kwa kuwa hiki ndicho chama tawala na Watanzania kama watawaliwa, wana haki ya kujua nini kinaamuliwa na chama tawala.

Jacob Daffi's picture

Zimwi la Richmond bado lamuandama Lowassa


Na Jacob Daffi - Imechapwa 02 November 2011

VIONGOZI waliokuwa serikalini wakati wa mkataba wa kuzalisha umeme wa dharula wa Richmond bado wanaendelea kung’ang’aniwa kwenye kashifa ya kushiriki kwenye ufisadi wa mkataba huo, MwanaHALISI limeelezwa.

Saed Kubenea's picture

Kikwete maji ya shingo


Na Saed Kubenea - Imechapwa 19 October 2011

RAIS Jakaya Kikwete amebakiwa na njia mbili tu kulinda nafasi yake katika Chama cha Mapinduzi (CCM).

Alfred Lucas's picture

Siri za Nape nje


Na Alfred Lucas - Imechapwa 31 August 2011

Ni zile zinazomhusu Lowassa
Profesa Mwandosya pia atajwa

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya taifa (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amejiingiza katika mradi wa kutafuta mrithi wa Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, imefahamika.

Jabir Idrissa's picture

Nape amgeukia Kikwete


Na Jabir Idrissa - Imechapwa 13 July 2011

NAPE Nnauye, katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) amemjia juu Rais Jakaya Jakaya Kikwete na kusema, “ni sehemu ya chimbuko la migawanyiko inayokikumba chama chake,” imeelezwa.

Saed Kubenea's picture

Kikwete hajamjibu Lowassa


Na Saed Kubenea - Imechapwa 06 July 2011

RAIS Jakaya Kikwete, ama ameshindwa au amekataa kujibu tuhuma za swahiba wake, kwamba serikali yake inaumwa ugonjwa wa kutofanya maamuzi magumu, MwanaHALISI limeelezwa.

Joster Mwangulumbi's picture

Mwisho wa maswahiba CCM


Na Joster Mwangulumbi - Imechapwa 06 July 2011

IPO mifano mingi ya kuonyesha namna viongozi marafiki wasivyoweza kutawala pamoja. Watapingana hadharani, watakorofishana na mwisho, mmoja hutafuta mbinu za kumpoteza mwingine kisiasa.

Mbasha Asenga's picture

Watumishi wanaugua posho, uvivu


Na Mbasha Asenga - Imechapwa 06 July 2011

TUJIULIZE maswali magumu leo. Hivi kama akina Edward Lowassa, Andrew Chenge na Rostam Aziz wakijivua nyadhifa zao zote ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakaachia ubunge wanaoshikilia kule Monduli, Bariadi Magharibi na Igunga, tutakuwa tumetatua matatizo ya kuzorota kwa utumishi wa umma?

Kondo Tutindaga's picture

Ni uamuzi mgumu, utapeli au ajali ya kisiasa?


Na Kondo Tutindaga - Imechapwa 06 July 2011

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amelidanganya tena Bunge. Amedai serikali ya awamu ya nne imefanya maamuzi mengi magumu kuliko serikali nyingine yoyote iliyotangulia. Hii ni kejeri ya aina yake na ninaamini rais mstaafu Benjamin Mkapa alipomsikia Pinda akitoa kauli hiyo alishikwa na bumbuwazi.

Saed Kubenea's picture

Lowassa amchokoza Kikwete


Na Saed Kubenea - Imechapwa 29 June 2011

EDWARD Lowassa, waziri mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, “amemtia kidole jichoni” Rais Jakaya Kikwete.

Saed Kubenea's picture

CCM watoana roho kwa urais


Na Saed Kubenea - Imechapwa 22 June 2011

RAIS Jakaya Kikwete ameendelea kukaa kimya huku viongozi wake wakianza “kutoana roho” kwa urais wa 2015, MwanaHALISI limeelezwa.

Alfred Lucas's picture

Lowassa amkatia rufaa Kikwete


Na Alfred Lucas - Imechapwa 15 June 2011

Atinga kwa Nabii Joshua kuombewa
Waziri Membe ateta na Rostam Aziz

EDWARD Lowassa, mwanasiasa anayetajwa “kujipanga kugombea urais mwaka 2015,” ametinga nchini Nigeria kufanya maombi, MwanaHALISI limeelezwa.

Saed Kubenea's picture

Lowassa, Rostam kumzima Kikwete


Na Saed Kubenea - Imechapwa 08 June 2011

Waahidi kumlipua vikaoni
CCM hatihati kuvunjika

HATUA yoyote ya Rais Jakaya Kikwete kutaka kuwafukuza ndani ya Chama Chaa Mapinduzi (CCM) wanaowaita “watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini,” yaweza kumuumiza mwenyewe, MwanaHALISI limeelezwa.

Jabir Idrissa's picture

Mafisadi CCM wageuka mbogo


Na Jabir Idrissa - Imechapwa 01 June 2011

Lowassa, Rostam wamkoromea Msekwa

SASA ni piga ni kupige ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wanakataa kujiuzulu, MwanaHALISI limeelezwa.

Kondo Tutindaga's picture

Ni ubaya wa Lowassa au udhaifu wa JK?


Na Kondo Tutindaga - Imechapwa 01 June 2011

KADRI siku zinavyosonga mbele, hali ya baadaye ya chama chetu – Chama Cha Mapinduzi (CCM) – ndivyo inavyozidi kutatanisha. Wanachama na wapenzi wa chama wamechanganyikiwa kwa sababu hawana kiongozi wanayeweza kumwamini ili awaelekeze waelekee wapi.

Saed Kubenea's picture

Mafisadi ‘kaa la moto’


Na Saed Kubenea - Imechapwa 11 May 2011

RAIS Jakaya Kikwete ameonyesha kutokuwa na uwezo wa kufukuza wenzake ambao wametuhumiwa ufisadi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

Mwandishi wetu's picture

CCM yafyata kwa mafisadi


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 04 May 2011

VIONGOZI wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameshindwa kuwaondoa katika chama hicho wale wanaowaita watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, imefahamika.

Ezekiel Kamwaga's picture

Lowassa, Rostam, Chenge bado


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 20 April 2011

PAMOJA na tambo za viongozi wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutaka kuwafukuza ndani ya chama hicho watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge, bado kimeshindwa kuwapa barua za kuwafukuza.