Makamba
Mlolongo wa Habari zinazomhusu Yusuf Makamba

Nape amepewa rungu kulipa kisasi
NGUMI za mitaani hazina sheria, kanuni, uwanja wala klabu za kujifunzia. Pambano linaweza kusababishwa na watu wawili, mara nyingi kwenye muziki au klabu za pombe. Kisa kinaweza kuwa bibi au bwana.
Ya Tambwe, Makamba na janga la CCM
MWALIMU Julius Nyerere alijaliwa na Muumba wake kuwa na njozi lakini pia kuona mbali. Baada tu ya kupata uhuru alitambua kwamba taifa lilikuwa linakabiliwa na maadui wakuu watatu, ujinga, maradhi na umasikini. Haijalishi sana kipi kinaanza na kinafuata kipi. Itoshe tu kusema aliona mbali.

CCM: Mwisho wa nyakati?
AGOSTI mwaka 2006, akiwa hata hajatimiza mwaka mmoja madarakani, Rais Jakaya Kikwete alipata mmoja ya mitihani yake ya kwanza.

Visa, vituko na filamu ya ziara ya Al-Adawi
WATUNZI wa filamu ni watu makini sana. Hupanga visa vikasisimua; huteua wahusika kulingana na nafasi zao; na huchagua maeneo ya kuigizia ili kusawiri kinachoelezewa na filamu yenyewe.

January Makamba ni wakala wa Dowans?
BABA wa Taifa Mwalimu Nyerere, katika moja ya hotuba zake alisema, ikulu ni mahali patakatifu. Alitumia neno ‘takatifu’ si kwa bahati mbaya. Kamusi inazungumzia neno hilo kama kitu kisichokuwa na dhambi, kilichotakasika.

Mafisadi wanatusingizia uhaini
WAZIRI mkuu Mizengo Pinda aliposema mafisadi ni hatari, wachambuzi wa masuala ya kisiasa walimrukia na kudai ni kauli ya kusalimu amri.

CCM hatarini kushitakiwa
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeingia katika mgogoro mpya na mwekezaji na huenda kikafikishwa mahakamani na hata kufilisiwa, imefahamika.

Kelele za udini ni ghiliba za watawala
Tangu mwaka 1995 Dk. Willibrod Slaa alipochaguliwa katika mazingira magumu ya kisiasa kuwa mbunge wa Karatu, hakuna mtu aliyemwangalia kama Mkatoliki.

Kiongozi aina ya Makamba ni janga la kisiasa
UKIMSIKILIZA mtu anayeitwa Yusuf Makamba, katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), huwezi kukwepa kufikia hitimisho kwamba madaraka ndani ya chama tawala yamerahisishwa sana.
Makamba zigo zito CCM
KAMA Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitakufa kabisa, Katibu Mkuu wake, Yusuph Makamba atapaswa kuwa mtu wa kwanza kuwajibika.

Dk. Slaa atishia Kikwete
VIGOGO wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wameokoa kampeni za uchaguzi kwa kukataa kuingia katika malumbano yanayohusu maisha binafsi ya wagombea, imefahamika.

Makamba: Hakuna atakayebaki salama
KUNA msemo wa kiswahili usemao, “Aliye katika nyumba ya kioo hatakiwi kurusha mawe nje.”

Serikali yafadhili kampeni za CCM
- Msemaji ikulu agoma kuongea
MABILIONI ya shilingi yatachotwa kutoka serikalini kugharamia kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

CCM itaazima wapi shoka lenye makali?
UKIMSIKILIZA Yusuf Makamba, katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kauli zake kuhusu tuhuma za rushwa katika mchakato wa kura za maoni za ubunge na udiwani ndani ya chama hicho, huwezi kukwepa kujenga hisia kwamba huenda anafunulia umma kujiandaa kwa hitimisho moja juu ya tuhuma hizi. Funika kombe mwanaharamu apite!

CCM wapata funzo kura ya maoni
HATA wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hawana hamu na chama chao. Wamerudisha kadi zao kwa viongozi wao.
‘Tumebaki na siasa za uchakachuaji’
CHAMA chochote cha siasa kikibinafsishwa na wafanyabiashara na kikajivua jukumu la ukombozi lililolengwa na waasisi wake, basi hugeuka kuwa moja wa maadui wa wananchi.

Makamba kumsifia Lipumba ni uchuro
UKIMUONA Yusuph Makamba, katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anasifia mwanasiasa mwenzake, ama chombo cha habari au mwandishi wa habari binafsi, basi jua hapo kuna jambo.

CCM haiwezi bila rushwa
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba anasema hakuna tatizo la kushtua wakati huu wanachama wakishiriki kura za maoni za kutafuta wagombea. Anasema mambo ni shwari.

Makamba apunguza kura CCM
YUSUF Makamba, katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), anatuhumiwa kupunguza kura za Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu wa Oktoba.
Makamba kumkana Kikwete?
KATI ya mwaka 1988 na 2001, jina la John Joseph Kamotho lilipamba vichwa vya habari vya magazeti nchini Kenya. Alikuwa Katibu Mkuu wa chama cha African National Union (KANU).

Kikwete awaangukia maaskofu
- Awatuma Malecela, Msekwa kuteta
- Wenyewe wazidi kutoa maelekezo
MISIMAMO mikali ya makanisa nchini imetikisa serikali na kufanya Rais Jakaya Kikwete kuomba huruma, MwanaHALISI limeelezwa.

Ikulu yaacha Rais, yatetea Makamba
TUMESIKIA watetezi wa Rais Jakaya Kikwete. Wanasema "Rais Kikwete hajageuzwa mradi."

'Luku' ya Makamba imedondoka
YUSUF Makamba, Mtendaji Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amepoteza "luku." Hajui lini ilidondoka na ilipodondokea. Tunaambiwa anahaha kuitafuta. Potelea mbali!

Lowassa, Rostam, wamvaa Makamba
HATUA ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Yusuph Makamba kwenda nyumbani kwa Spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta, imeudhi baadhi ya vigogo waandamizi wa chama hicho, MwanaHALISI limeelezwa.
Makamba ana ajenda gani?
YUSUPH Makamba, katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ana ajenda gani dhidi ya Spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta?

Yusuf Makamba: Mara joto, mara baridi...
TABIA ya Yusuf Makamba, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni ileile ya mara baridi, mara joto, mara vuguvugu na mara baridi, tena katika muda mfupi.

Sitta afanywa kondoo wa kafara
SPIKA wa Bunge, Samwel Sitta ameshikiwa bango na wapinzani wake wa kisiasa wakishinikiza afukuzwe katika chama kutokana na msimamo wake wa "kujenga Bunge lenye kasi viwango."

Hukumu ya Makamba: Makamba, Londa washiriki Rushwa
MwanaHALISI ndilo gazeti pekee ambalo liliandika na kung'ang'ania ufuatiliaji wa madai ya Mbunge Halima Mdee

Makamba kinara wa uongo Biharamulo
- Atumia ubabe wa CCM kutishia wapiga kura
NGWE mpya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kueneza uwongo imewadia. Kiongozi mkuu katika hili ni yuleyule, Yusuph Makamba, katibu mkuu wa chama hicho.

Makamba, Londa roho juu
UAMUZI juu ya shauri lililofunguliwa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Yusuph Makamba na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Salum Londa dhidi ya mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee (Chadema), unatarajiwa kutolewa katika mkutano wa Bunge ulioanza hapa jana, imefahamika.