Mkapa
Mlolongo wa Habari zinazomhusu Benjamin Mkapa

Mkapa anasimangwa kwa mafao haya
NILIPOANDIKA mwezi uliopita ubaya wa viongozi wakuu wastaafu wa aina ya Benjamin Mkapa, kufanya kampeni majukwaani kutetea chama tawala, na kupendekeza wafutiwe mafao, nilipata meseji kedekede, zikiashiria kuniunga mkono.
Hoja yangu ilikuwa kwamba kauli za rais mstaafu Mkapa jimboni Arumeru Mashariki wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo mwezi uliopita, zilimshusha hadhi, na alivyokuwa akiwaandama baadhi ya Watanzania wanaogharamia mafao yake.

Mkapa kubali makosa uliyofanya
BENJAMIN Mkapa inabidi aanze kukubali makosa ya utawala wake. Akubali kuwa maamuzi mbalimbali aliyochukua yamechangia kulifikisha taifa letu hapa lilipo, hivyo asikae katika wingu la udanganyifu kuwa sera zake zilikuwa nzuri kwa taifa.
Akizungumza katika kongamano la Kigoda cha Mwalimu Nyerere, kati ya mengi aliyozungumzia Mkapa huku aking’aka, alisema kushindwa kwa sera ya ubinafsishaji kuokoa viwanda vyetu vilivyobinafsishwa (hata kama si vyote) siyo “tatizo” lake.

CHADEMA kufuta kinga ya Mkapa
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimebainisha maeneo matano ya kipaumbele katika “kipindi kifupi kijacho,” ili kujiimarisha miongoni mwa umma.

Mkapa ashukuru Mungu hakuwa Mara
RAIS mstaafu Benjamin Mkapa kafanya kosa kubwa sana. Matusi ya reja reja aliyoyatoa Arumeru Mashariki angeyatamka popote pale mkoani Mara iwe Zanaki, Ikizu, Ikoma, Bunchari, Nyabasi, Nyamongo, Bukira, Bwiregi, Busweta au Ngoreme angesababisha balaa kubwa.
Mtu hawezi kutukana ukoo mkoani Mara na wanaukoo wakamwachia hivi hivi. Hapana haiwezekani, utapigwa kwa marungu na mapanga mpaka “nzi wakukatae” yaani hadi usitamanike.

CCM ndio wavivu wa kufikiri
NDIVYO alivyo Rais mstaafu Benjamin William Mkapa. Akitaka kujisafisha kutokana na tuhuma nzito zinazomkabili, hudai “watu wavivu wa kufikiri na hufanya mambo kwa hisia.”

Mkapa, Kingunge acha kulalama
NI msimu wa malalamiko. Kila mmoja ni mlalamishi. Rais Jakaya Kikwete analalamika. Mtangulizi wake, Benjamin Mkapa analalamika.

Mkapa: Anakwenda Igunga kuvuna aibu
PAMOJA na majigambo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwamba kitashinda uchaguzi mdogo wa ubunge jimboni Igunga, mkoani Tabora, Rais mstaafu Benjamin Mkapa anayekwenda kuzindua kampeni zake anaweza kuvuna aibu.

Wangeanza hawa taifa lingekuwaje?
MASHAMBULIZI dhidi ya Mwalimu Julius Nyerere yameendelea kwa nguvu katika mitandao ya intaneti. Binafsi, siamini kuwa wanaochafua Nyerere wametumwa na watawala.

Kikwete kuitwa mahakamani
RAIS Jakaya Kikwete ametajwa kuwa mmoja wa mashahidi “muhimu sana” wa Profesa Costa Ricky Mahalu anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi.

Mkapa kutinga kortini
- Ni katika kesi ya Prof. Mahalu
- Ikulu yahaha kumwokoa Kikwete
HATIMAYE rais mstaafu Benjamin William Mkapa atatinga mahakamani mjini Dar es Salaam.

Mkapa kalewa au kapotoka?
RAIS mstaafu Benjamin Mkapa si mtu anayependa kusema au kuhojiwa, lakini pale anapofanya hivyo huzua kasheshe na kauli yake kulalamikiwa.

Mkapa, Malecela, Sumaye wamkimbia Kikwete
VIGOGO waastafu ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali, wamekacha kampeni za mgombea urais Jakaya Kikwete, MwanaHALISI limeelezwa.

Mkapa akianza, serikali ikimbie
MATUKIO mawili yanatarajiwa kubadilisha mwelekeo wa kiuchumi wa eneo la mashariki mwa Bara la Afrika katika siku za usoni.

Kiwewe kitupu CCM
KOMBORA lililorushwa na muasisi wa mageuzi nchini, wakili wa mahakama kuu, Mabere Marando limetia kiwewe Rais Jakaya Kikwete na baadhi ya wasaidizi wake, MwanaHALISI limeelezwa.

Nani amelonga taifa hili?
MWAKA mmoja uliopita, Tanzania ilikuwa nchi ya tatu barani Afrika kwa kuzalisha kiasi kikubwa cha dhahabu.

Tumekwama, turejee kwa Nyerere
HUU ni mwaka wa uchaguzi. Ni uchaguzi mkuu wa nne kufanyika nchini tangu kuzikwa kwa udikteta wa mfumo wa chama kimoja miaka 18 iliyopita.

Rada kumuumbua Mkapa
- Lipumba ataka Bunge lichunguze
- Hata dili za helikopta na ndege ya rais
BAADA ya kampuni iliyouza rada kwa serikali kukiri kutumia rushwa, Bunge limeombwa kuchunguza mikataba yote mikubwa inayomuhusisha mfanyabiashara Sailesh Vithlan.

Mkapa unavuna ulichopanda
RAIS mstaaafu Benjamin Mkapa anajifanya hamnazo. Anatuhumu na kushutumu wananchi na vyombo vya habari, kwamba anasakamwa bila makosa.

Haya ni ya kwako Ben Mkapa
RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, aliyetegemea mno nchi wafadhili kuongoza serikali kipindi chote alichodumu Ikulu, analalamika.

Kikwete ni zaidi ya Mkapa na Mwinyi
MAKALA sita zilizochapishwa mfululizo katika MwanaHALISI wiki tano zilizopita, ndizo zilizonisukuma kupata ujasiri wa kumtetea Rais Jakaya Kikwete, dhidi ya hoja za wapinzani wake wa kisiasa.

Njia ya Chiluba, Muluzi bado yamsubiri Mkapa
KUPAMBANA katika kufunika kashfa za ufisadi au kujaribu kutosa wale ambao waweza kuonekana kondoo wa kafara kumeshamiri kipindi cha utawala wa awamu ya nne.

Tukatae kuwa taifa la ovyo
WATANZANIA tumeamua kuwa taifa la watu wa ovyo! Ni watu wa ovyo hasa. Kutotaka kutenda kwa kufuata sheria wala taratibu katika taifa linalojivuna kwa umaarufu miongoni mwa mataifa yanayoendelea, ni kitu cha ovyo kabisa.

Mkapa atishia serikali
- Watetezi wake wajipanga upya
- Watuhumiwa ufisadi wamo
MPANGO wa kumtetea rais mstaafu Benjamin Mkapa umelenga mbali. Umeandaliwa mahsusi kubeba wote wanaolalamika kuwa Rais Jakaya Kikwete amewatelekekeza, MwanaHALISI limeelezwa.

Pinda: La Mkapa limekushinda
UTETEZI wa rais mstaafu wa Benjamin Mkapa ambao ulifanywa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akihitimisha mjadala wa bajeti ya ofisi yake, Ijumaa iliyopita, haukubaliki.

Sakata la Mkapa: Vyombo vya habari vimetimiza wajibu wake
HATIMAYE kazi ya vyombo vya habari imeonekana. Kumbe king’ang’anizi kina manufaa yake na hasa ndilo jukumu la uandishi wa habari.

Mkapa kikaangoni
- Achota mabilioni NSSF
- Ashindwa kuyarejesha
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amemwanika rais mstaafu, Benjamin Mkapa kwa kuonyesha kuwa alitumia vibaya fedha za mkopo kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Bethidei ya Anna Mkapa na njozi zangu
LEO 29 Aprili, Anna Mkapa anatimiza miaka 67. Ni yule mke wa rais mstaafu Benjamin Mkapa aliyekuwa mpangaji wa ikulu kati ya 1995 na 2005.

Mkapa aangukia Kikwete
- Akutana na vigogo kuomba msaada
- Tuhuma mpya zazidi kumuandama
RAIS mstaafu Benjamin Mkapa amelalamika kuwa anasakamwa na wanasiasa na anachafuliwa, MwanaHALISI limeambiwa.

Benjamin Mkapa presha juu
BAKILI Muluzi, rais wa zamani wa Malawi anakabiliwa na mashitaka 80 ya rushwa na kujipatia mali ya umma visivyo.

Sabuni ya Mbilinyi haimsafishi Mkapa
- Mbilinyi atetea Mkapa, azamisha mkewe
WAZIRI wa Fedha wa zamani katika serikali ya Awamu ya Tatu, Profesa Simon Mbilinyi, amejitosa katika mjadala unaomhusisha rais mstaafu Benjamin Mkapa.