Pinda
Mlolongo wa Habari zinazomhusu Waziri Mkuu Pinda
Mbio za urais zaingia kanisani
- Lowassa tayari ashika mwaliko wa 2013
- Sitta, Membe wapigana vikumbio
- Mbowe: Mimi hasitaki urais
MAKADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kutaka urais mwaka 2015, wameanza mbio katika nyumba za ibada, MwanaHALISI imebaini.

Pinda ahalalisha uhalifu mkoani Mara
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, wiki iliyopita alifanya ziara mkoani Mara ambako pamoja na mambo mengine aliagiza na kuelekeza kwamba wakazi wa mkoa huo unaogubikwa na vurugu na mapigano ya mara kwa mara watumie mabaraza ya jadi maarufu kama iritongo kutatua migogoro yao.
Kama mnajua, epusheni balaa
WIKI iliyopita Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alionya kwamba kuwepo kwa viongozi wengi wasio waadilifu, wenye uchu wa mali na wanaojilimbikizia mali nchini kunahatarisha amani na utulivu.

Pinda naye ‘Kassim wa Matumizi’
OFISI ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda imetumia zaidi ya Sh. 174.5 milioni kwa kile ambacho kimeelezwa kuwa “mchakato wa kufanikisha bajeti yake,” MwanaHALISI limeelezwa.

Posho na umasikini wa ‘kutaga mayai’
KAULI ya waziri mkuu Mizengo Pinda, kwamba serikali “itaangalia upya suala zima la posho,” inaelekea kuzima joto la hoja muhimu.
Pinda, amesahau ‘wazazi’ wake
NIMEJITOSA mjadala wa posho za wabunge baada ya kuona upotoshaji mkubwa uliofanywa na waziri mkuu wa Jamhuri, Mizengo Pinda.

Pinda anatutuliza huku anatuumiza?
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ametufungua macho wengi. Hili limejidhihirisha wakati akihitimisha mjadala wa bajeti ya ofisi yake bungeni, mwishoni mwa wiki iliyopita.
Ni uamuzi mgumu, utapeli au ajali ya kisiasa?
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amelidanganya tena Bunge. Amedai serikali ya awamu ya nne imefanya maamuzi mengi magumu kuliko serikali nyingine yoyote iliyotangulia. Hii ni kejeri ya aina yake na ninaamini rais mstaafu Benjamin Mkapa alipomsikia Pinda akitoa kauli hiyo alishikwa na bumbuwazi.
Unafiki wa CHADEMA, ulafi wa CCM
TAKRIBANI majuma mawili sasa, Bunge la Jamhuri na baadhi ya vyombo vya habari nchini vimetawaliwa na mjadala wa posho za wabunge na watumishi wa serikali.

Pinda ameanza kunogewa na madaraka
SIKU moja nilikuwa najadiliana na rafiki yangu juu ya mustakabali wa taifa hili hasa tunapowatazama viongozi wa kisiasa. Pamoja na mengi aliyonieleza, kitu kimoja hadi leo ninakikumbuka.

Nyuma ya pazia la posho za wabunge
SIKU 68 tangu Mizengo Kayanza Peter Pinda ateuliwe kuwa waziri mkuu kuchukua nafasi ya Edward Lowassa alikumbana na mtihani wa kwanza mgumu, kumkalisha chini waziri wake na kumwambia ajiuzulu.
Spika Makinda na ‘kiatu pwayu’
NAUNGANA na wanaosema Spika Anne Makinda hana uwezo wa kuongoza bunge; hasa bunge la sasa. Chombo hiki kikuu nchini – Bunge – kina majukumu matatu makuu: kutunga sheria, kushauri na kusimamia serikali na kuwakilisha wananchi.

CHADEMA yaumbua Pinda
- Yataka afute kauli yake bungeni
- Hatima yake mikononi mwa spika
- Spika Makinda kumfichia aibu
USHAHIDI wa CHADEMA, kuthibitisha jinsi Waziri Mkuu Mizengo Pinda “alivyodanganya bunge,” umesheheni vielelezo ambavyo vinaweza kumjeruhi kisiasa – yeye binafsi na serikali yake.

Pinda aetembea na kiziba mdomo
RAIS Yoweri Museveni wa Uganda wiki mbili zilizopita alilazimika kuzozana na vyombo vya habari hasa gazeti moja lililochora katuni inayomhusu.

Pinda atajwa mauaji Arusha
JITIHADA za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuepusha maafa mjini Arusha, zilihujumiwa na serikali, MwanaHALISI limeelezwa.

Mnamlinda Pinda au mna lenu jambo?
KATIKA lugha ya Kifaransa, kuna maneno ambayo mtu hatakiwi kuyasema hadharani. Mojawapo ni neno Merde. Hata hivyo, baada ya kusikia kilichotokea katika Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es Salaam Ijumaa iliyopita, nilishindwa kujizuia kusema neno hilo.

Wezi wa Dowans hawa
MAFISADI watatu waliojipanga kuchota Sh. 185 bilioni kutoka serikalini, zikiwa fidia kwa kuvunja mkataba wa kampuni ya kufua umeme ya Dowans, wamefahamika.
Tunapigania haki ya wote
SASA serikali imepitiliza katika kunyanyasa gazeti hili. Ijumaa iliyopita, mwandishi wetu, Saed Kubenea, alizuiwa kuingia mkutanoni Ikulu.

Pinda akimbia MwanaHALISI
SERIKALI imezuia mwandishi wa MwanaHALISI kuhudhuria mkutano wa vyombo vya habari ulioitishwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Nani anayekabidhiwa fedha ya Dowans?
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri, Mizengo Pinda amejitwisha zigo lisilobebeka. Litamuangusha. Ameahidi kulipa mabilioni ya shilingi kwa kampuni ya kufua umeme wa dharula, Dowans Holding Tanzania Limited.

Pinda ni shokabuzoba ya serikali ya JK
KATIKA gari kuna chombo kiitwacho shock absorber (shokabzoba); madereva mitaani wanaziita ‘shokap’. Kazi kubwa ni kuongeza mneso wa gari na kupunguza mtikisiko mkubwa likiingia kwenye mashimo mashimo au barabara mbovu.

Pinda, Waziri Mkuu muungwana au dhaifu
UNAPOZUNGUMZA viongozi wakuu wa kitaifa nchini, unakusudia Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu kwa upande wa utawala, lakini pia yumo Jaji Mkuu kwa upande wa Mahakama na Spika wa Bunge kwa upande wa Bunge.

Pinda kupandishwa kizimbani
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda huenda akaburuzwa mahakamani wakati wowote kuanzia sasa, imefahamika. Hatua hiyo inaandaliwa na wakazi wa kijiji cha Mgusu, kata ya Mtakuja, Geita mkoani Mwanza

Kumbe Pinda naye ana usanii
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Tabora mwishoni mwa wiki, alitoa kauli yenye utata alipokuwa kwenye jimbo la Igunga, ambalo mbunge wake ni Rostam Aziz.

Pinda ametangaza 'umasikini'
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ametangaza "umasikini" wake na hakuna aliyemwamini, ikiwa ni pamoja na yule aliyemuuliza swali.

Mizengo Pinda: Siamini katika mali
NI takribani saa sita kasorobo, Alhamisi iliyopita. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda anaingia katika ukumbi wa mikutano wa ofisi yake, Magogoni, Dar es Salaam akiwa amevalia suti nyeusi maarufu kwa jina la "Kaunda."

Pinda akumbana na 'madudu' ya Lowassa
MABILIONI ya shilingi za walipa kodi, ambayo Edward Lowassa alishinikiza yalipwe kwa kampuni ya kutengeneza matairi ya General Tyre (GT), yameteketea.

Mtoto wa mkulima ameanza kupoteza imani
NAANZA kuhofu kwamba Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameanza kufuta ile imani ambayo Watanzania wengi walikuwa wamempa baada ya kujitambulisha kama mtoto wa mkulima, mara tu baada ya kuteuliwa kushikwa wadhifa huo Februari mwaka jana.

Pinda: La Mkapa limekushinda
UTETEZI wa rais mstaafu wa Benjamin Mkapa ambao ulifanywa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akihitimisha mjadala wa bajeti ya ofisi yake, Ijumaa iliyopita, haukubaliki.

Nani atafuata nyayo za Pinda?
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Mizengo Pinda, amejiandikia historia kwa kufanya mambo mawili makubwa.