Rostam
Mlolongo wa Habari zinazomhusu Rostam Aziz

Rostam Aziz anacheza kama Pele
ROSTAM Aziz, kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyejiuzulu nyadhifa zake zote katika CCM kwa madai ya kuchoshwa na siasa uchwara, anajua kucheza kama Pele na kupanga mipango na mikakati kama Kanisa Katoliki.

Rostam, Lowassa hawafukuziki
ROSTAM Aziz, mwanasiasa, mfanyabiashara na mmoja wa maswahiba wa karibu wa Rais Jakaya Kikwete, hafukuziki ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

Ukiua ufisadi utakuwa umeua CCM
ILIPOTANGAZWA kuwapo kwa mradi wa kujivua gamba ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baadhi yetu tulitabiri mapema kwamba hizo ni ghiliba na pengine ni sehemu ya sherehe za kuadhimisha miaka 34 ya kuzaliwa kwa CCM.
CCM: Kutema tamu, kumeza chungu
KAMPENI za uchaguzi mdogo katika jimbo la Igunga, mkoani Tabora zinatarajiwa kuanza mjini humo Alhamisi wiki hii. Tayari viroja vya wanasiasa vimeanza na anayetegemea kuona au kusikia matumizi ya akili huko Igunga anajisumbua. Huu utakuwa mwezi wa kupumzisha akili na ukweli, kisha kutumia unafiki na uwongo ili kunogesha siasa za nchi yetu.
Kwa hali ilivyo ni mchuano kati ya CHADEMA na vyama vingine.
Mkapa: Anakwenda Igunga kuvuna aibu
PAMOJA na majigambo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwamba kitashinda uchaguzi mdogo wa ubunge jimboni Igunga, mkoani Tabora, Rais mstaafu Benjamin Mkapa anayekwenda kuzindua kampeni zake anaweza kuvuna aibu.

Sitta, Rostam wapasua CCM Igunga
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinaingia katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga mkoani Tabora, kikiwa kimekatika vipande viwili, imefahamika.

JK amuangukia Rostam
RAIS Jakaya Kikwete sasa anapanga kumuangukia aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, MwanaHALISI limeelezwa.

Rostam ‘ajichimbia’ Ulaya
ROSTAM Aziz, aliyejiuzulu uongozi wa siasa, ametajwa kuwa nchini Uswisi kwa kinachodaiwa kuwa “safari ya mapumziko,” MwanaHALISI limeelezwa.

Filamu mpya ya Rostam Aziz
TUKIO la kujiuzulu nyadhifa zake zote Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz linafanana sana na alichofanya aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kilombero, Abbas Gulamali.

Huyu anajua ‘machungu’ ya Rostam
HATIMAYE Rostam Adulrasul Aziz ameandika historia. Ni kwa kujiuzulu nafasi zake zote ndani ya chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hatuna sababu ya kumpongeza Rostam
SIKUBALIANI na wanaopongeza uamuzi wa aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, kwa kujiuzulu. Nawakatalia zaidi wale wanaodai amefanya hivyo kwa maslahi ya taifa.

Nape amgeukia Kikwete
NAPE Nnauye, katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) amemjia juu Rais Jakaya Jakaya Kikwete na kusema, “ni sehemu ya chimbuko la migawanyiko inayokikumba chama chake,” imeelezwa.

Watumishi wanaugua posho, uvivu
TUJIULIZE maswali magumu leo. Hivi kama akina Edward Lowassa, Andrew Chenge na Rostam Aziz wakijivua nyadhifa zao zote ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wakaachia ubunge wanaoshikilia kule Monduli, Bariadi Magharibi na Igunga, tutakuwa tumetatua matatizo ya kuzorota kwa utumishi wa umma?

Lowassa amkatia rufaa Kikwete
- Atinga kwa Nabii Joshua kuombewa
- Waziri Membe ateta na Rostam Aziz
EDWARD Lowassa, mwanasiasa anayetajwa “kujipanga kugombea urais mwaka 2015,” ametinga nchini Nigeria kufanya maombi, MwanaHALISI limeelezwa.

Lowassa, Rostam kumzima Kikwete
- Waahidi kumlipua vikaoni
- CCM hatihati kuvunjika
HATUA yoyote ya Rais Jakaya Kikwete kutaka kuwafukuza ndani ya Chama Chaa Mapinduzi (CCM) wanaowaita “watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini,” yaweza kumuumiza mwenyewe, MwanaHALISI limeelezwa.

Mafisadi CCM wageuka mbogo
- Lowassa, Rostam wamkoromea Msekwa
SASA ni piga ni kupige ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wanakataa kujiuzulu, MwanaHALISI limeelezwa.
Malipo Dowans ni marafiki wanaolipa marafiki
RAIS wangu tukubali kuwa kikombe cha Babu Mchungaji Ambilikile Mwasapile wa Sumunge, Loliondo kinatibu maradhi mengi kuliko aliyoyataja na anayoyafahamu.

Mafisadi ‘kaa la moto’
RAIS Jakaya Kikwete ameonyesha kutokuwa na uwezo wa kufukuza wenzake ambao wametuhumiwa ufisadi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

CCM yafyata kwa mafisadi
VIONGOZI wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameshindwa kuwaondoa katika chama hicho wale wanaowaita watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, imefahamika.

Lowassa, Rostam, Chenge bado
PAMOJA na tambo za viongozi wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutaka kuwafukuza ndani ya chama hicho watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge, bado kimeshindwa kuwapa barua za kuwafukuza.

CCM wamevua gamba, wameacha sumu
UNAFIKI haujengi. Migogoro mingi serikalini, vyama vya siasa, vya kiraia na mitaani husababishwa na unafiki. Hili ndio moja ya magamba yanayokitesa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kikwete atajwa mradi wa kuua magazeti
RAIS Jakaya Kikwete ameombwa kuminya kiuchumi vyombo vya habari binafsi ili kuimarisha vijarida vitakavyoanzishwa na umoja wa vijana wa chama chake (UV-CCM), MwanaHALISI limegundua.

Furaha ya Rostam kuzimwa?
SHIRIKA la umeme la taifa (TANESCO) limetupa kete muhimu likilenga kusimamisha ulipaji tozo ya Sh. 94 bilioni kwa mbunge wa Igunga na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC-CCM), Rostam Aziz kupitia kampuni ya Dowans Holdings SA, MwanaHALISI limeelezwa.

Rostam aingiza mkenge TANESCO
MPANGO wa wamiliki wa kampuni ya Dowans kuizunguka serikali na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ili kujinufaisha kiuchumi umegundulika.

‘Mafisadi’ wanakumbatiwa, watetezi wanadhihakiwa!
NIMEPITIA kitabu cha Zaburi nikakutana na maneno: “Kama misingi ikiharibika, mwenye haki atafanya nini?” Hicho ndicho tunachokishuhudi leo nchini. Misingi ya taifa inabomolewa kwa kasi, huku waadilifu, wazalendo, na wanaolitakia mema taifa wanaulizwa, “Mtafanya nini?”

Siri ambayo Al adawi ameificha
KUNA siri moja kubwa ambayo anayejiita mmiliki wa Dowans, Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi, hataki kuizungumzia katika mkakati wake wa kushinikiza serikali kununua mitambo yake, ama kuikodisha.

Dowans rushwa tupu
- Siri za mawakili wao zavuja
- Wahofia TANESCO kushinda
Taarifa zinasema hoja ya kuwapo rushwa katika mkataba kati ya Dowans na TANESCO zilitosha kuishawishi Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), kutupilia mbali madai ya kampuni hiyo.

Misingi ya kutaifisha Dowans hii
KUNA hoja mbili kuu za kisheria zinazoweza kutumika kutaifisha mitambo ya kampuni ya kufua umeme ya Dowans. Kwanza, kutaifisha kwa kulipa fidia. Pili, kutaifisha bila kulipa chochote.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imeweka “Malengo muhimu na misingi ya mwelekeo wa shughuli za serikali kuwa ni pamoja na ustawi wa wananchi.”
Katiba pia imewapa wananchi haki mbalimbali na wajibu. Kwa mfano, ibara ya 24(1) ya katiba inatoa haki ya kumiliki mali na hifadhi ya mali hiyo na “...

Rostam aiweka serikali mfukoni
ANAYEJIITA mmiliki wa makampuni ya Dowans ametua nchini kibabe kwa shabaha ya kutisha serikali, MwanaHALISI limeelezwa.
Mmiliki Dowans aja na mazingaombwe
BRIGEDIA Jenerali mstaafu, Suleiman Mohammed Yahya Al Adawi, anayetajwa kuwa mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya Dowans Holdings SA ameongeza utata nchini.