MKUTANO ulioitishwa na viongozi wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) juzi Jumatatu kama jitihada za kutafuta ufumbuzi wa mgawanyiko mkubwa unaokikabili chama hicho umeshindwa kujenga msingi wa usuluhishi, MwanaHALISI limeelezwa.
Mlolongo wa Habari zinazomhusu Samwel Sitta
Kubenea asema, Sitta mwongo
MKURUGENZI mtendaji wa gazeti la MwanaHALISI, Saed Kubenea, amekana tuhuma kwamba gazeti lake “limenunuliwa na watuhumiwa wa ufisadi nchini.”
Sitta ‘kanyea kambi’
SAMWEL Sitta ametuhumu gazeti hili, kuwa linatumiwa na watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini ili “kumchafua” yeye na wenzake.

Sitta, Rostam wapasua CCM Igunga
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinaingia katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga mkoani Tabora, kikiwa kimekatika vipande viwili, imefahamika.

Sitta na dhambi ya unafiki ndani ya CCM
NIMEKUWA nikimsifu Samwel Sitta anaposimama kueleza, kujadili na kutetea anachokiamini. Huwa namsifu mwanasiasa huyu mwerevu kwa sababu huwa anaeleza kwa msisitizo, nguvu na mvuto mkubwa hicho anachokiamini.

Waziri Sitta ‘anakaa kwa Makinda?’
WAZIRI wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta amekuwa sehemu ya mjadala bungeni. Ni kuhusu nyumba iliyokodishwa na serikali kwa ajili ya makazi maalum ya spika wa bunge.

Spika Makinda, kazi kwako!
FEBRUARI 6, 2008, Spika wa Bunge la 9 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyekuwa Spika wa Bunge, Samweli Sitta alitoa dokezo zito kuhusu naibu wake Anne Makinda.
‘Waasisi wa CCJ wafukuzwe CCM’
TANGU taarifa kwamba spika wa zamani wa Bunge, Samwel Sitta na Dk. Harrison Mwakyembe, ni miongoni mwa viongozi waandamizi wa Chama cha Jamii (CCJ) ziibuke, mjadala mkubwa umekuwepo ndani na nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Sitta, Dk. Mwakyembe hawatoki CCJ - Ng’hily
ANAJIAMINI na anasema anaweza kusimamia kile anachokiamini.
Makala ya Mtangazaji – Porokwa
Kwa muda wa takribani wiki mbili sasa, vyombo vya habari vimeripoti maelezo yaliyotolewa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA, Mh. Anthony Komu, kwamba Nape Nnauye alikuwa mwasisi wa Chama Cha Jamii (CCJ).

‘Sitta, Mwakyembe watoswe’
- Ni kwa ‘usaliti mkuu’ ndani ya CCM
- Lowassa, Rostam, Chenge nao wafukuzwe
TUHUMA za kukisaliti chama zinazowakabili spika wa zamani wa Bunge, Samwel Sitta na mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, zaweza kuwafukuzisha kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

Kikwete ndani ya CCJ
NYOTA ya spika wa zamani wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta imezimwa, MwanaHALISI limeelezwa.

Mwakyembe na wapambanaji wenzake wangefanyaje
KUNA mjadala umeibuka katika siku za karibuni tangu Rais Jakaya Kikwete alipowateua Samwel Sitta na Dk. Harrison Mwakyembe kwenye baraza la mawaziri.

Nani anasema Sitta kashushwa?
MOJA ya mijadala mikubwa inayoendelea nchini kwa sasa katika vyombo vya habari ni kuhusu aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta kuteuliwa kuwa Waziri wa Afrika Mashariki.

Sitta amtikisa Kikwete
HATUA ya kumuengua aliyekuwa spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta kwenye kinyang’anyiro cha uspika, ililenga kusafishia njia aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, MwanaHALISI limeelezwa.

Chenge ataka kuunajisi uspika
TANZANIA ingekuwa ni nchi inayojali japo kwa chembe tu uadilifu, mtu kama Andrew Chenge hasingethubutu kuwania nafasi yoyote ya kuchaguliwa na wananchi. Kikubwa ambacho angelikifanya ni kuendesha biashara zake.

Sitta kung'olewa?
KUJITOSA kwa Andrew Chenge, katika mbio za kuwania nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri, kumelenga kumuengua Samwel Sitta aliyeshika kiti hicho kwa miaka mitano iliyopita.
Sura mbili tofauti za Samwel Sitta
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyemaliza muda wake, Samwel Sitta ameomba “kuvaa viatu” vya Jakaya Kikwete kupambana na Dk. Willibrod Slaa katika mdahalo juu ya utoaji elimu na afya bure kwa wananchi.
Sitta atavuna aibu tupu kwa Dk. Slaa
MGOMBEA ubunge jimbo la Urambo, Samwel Sitta, anatafuta aibu. Anadai kuwa anataka mdahalo na Dk. Willibrod Slaa.

Spika Sitta ameweka viwango, mwingine nani?
BUNGE la kwanza la serikali ya Rais Jakaya Kikwete linamaliza muda wake wiki hii na kama kuna nafasi ambayo ilipewa maana mpya na Bunge hilo, basi ni ile ya Spika wa Bunge.

Sitta kung’olewa uspika
KUNA njama za kuwatoa “kafara” wabunge 15 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ili kusafisha njia ya urais wa Edward Lowassa, MwanaHALISI limeelezwa.

Sakata la Richmond: Sitta aachwe, abanwe Kikwete
KUNA viumbe viwili vya ajabu sana lakini kwa namna fulani vinafanana - kinyonga na kasuku. Kinyonga ameumbwa na uwezo wa kubadilika rangi kulingana na mazingira.

Sitta alivyogeuka 'jiwe la chumvi'
SABABU za Spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta kuamuru bunge kufunga mjadala wa Richmond ni nyingi.

Richmond: Kufunga mjadala bungeni ni kukejeli umma
BUNGE la Jamhuri limetishwa. Spika Samwel Sitta “ameng’olewa meno” na kurejeshwa katika “dini” yake ya asili.

'Mitume kumi na mbili' imevuna au imepoteza?
- SAKATA LA RICHMOND
HOJA za msingi hazijajadiliwa. Watuhumiwa wa ufisadi wameendelea kupeta. Vidonda vya migawanyiko vilivyokuwa vipate tiba, vimeshindikana kupona.

Mpango wa kumfukuza Sitta waiva
KUMEKUCHA. Juhudi za kumfukuza Spika wa Bunge Samwel Sitta kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimeanza upya, MwanaHALISI limeelezwa.

Nyumba ya Kikwete inaungua
KAMATI ya rais mstaafu Ali Hassani Mwinyi iliyoundwa kutafuta "kiini cha uhasama" miongoni mwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), imezidisha nyongo.

Sakata la Posho mbili: Tatizo sheria zisizo za haki
NAOMBA kupanua mjadala kuhusu wabunge na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) juu ya dhana nzima ya utawala wa sheria.

Mkakati wasukwa kumwangusha Spika Sitta
BAADA ya kukwama kwa jaribio la kwanza la kumng'oa Spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta mjini Dodoma kupitia chama chake, sasa la pili linadaiwa kuandaliwa kwa ustadi.

Lowassa, Rostam, wamvaa Makamba
HATUA ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Yusuph Makamba kwenda nyumbani kwa Spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta, imeudhi baadhi ya vigogo waandamizi wa chama hicho, MwanaHALISI limeelezwa.
