CHADEMA
Mlolongo wa Habari za Chama cha Demokrasia na Maendeleo

Regia alifanya mengi makubwa
REGIA Estelatus Mtema hatunaye; ametutoka ghafla na kuacha majonzi. Ajali mbaya aliyopata saa 5.30 hivi Jumamosi iliyopita eneo la Ruvu mkoani Pwani ndiyo imepora maisha yake. Anatarajiwa kuzikwa kwao Ifakara, Kilombero.
Wazazi wanalia, ndugu na jamaa wanalia; waliokua, kusoma, kufanya kazi naye wanasikitika. Wanasiasa hasa wanachama, wafuasi na viongozi wa chama chake – Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wanaombeleza kumpoteza mbunge huyo kijana na mpambanaji.

Opulukwa: Nipo vitani Meatu, nitashinda
MBUNGE wa jimbo la Meatu, Meshack Opulukwa anapiga mayowe. Kwa miezi miwili hakuna anayemsikiliza. Amekuwa akihangaika kutafuta ufumbuzi baada ya serikali ya mkoa kuamuru operesheni ya kuhamisha kwa nguvu makazi ya watu katika kijiji cha Mwangudo, ndani ya jimbo analoliwakilisha.
Uhamishaji huo umefanywa kwa sababu ya kinachoelezwa wananchi “wanaishi ndani ya hifadhi ya jamii ya Makao.” Matokeo ya operesheni hiyo ni kuteketezwa kwa moto zaidi ya nyumba 1,000 za wananchi na mamia ya watu kuumia.

Kikwete akaliwa kooni
- Naye atakiwa kujiuzulu
- Waraka mzito wavuja
- CHADEMA yaitwa ‘mchawi’
RAIS Jakaya Kikwete amekaliwa kooni. Wakati chama chake kinakabiliwa na wimbi la kukimbiwa na wanachama na viongozi, swahiba wake anashikilia kuwa wenye “tuhuma za ufisadi” wajiuzulu kama yeye.

Waziri kumkimbia Lowassa CCM
WAZIRI mmoja mwandamizi ndani ya serikali ya Rais Jakaya Kikwete, yuko mbioni kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM), imefahamika.
CHADEMA yatikisa Ikulu
RAIS Jakaya Kikwete hakufahamu kwa undani kilichomo kwenye muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba (Constitutional Review Bill 2011), uliopitishwa na bunge hivi karibuni, MwanaHALISI limeelezwa.
CCM: Kutema tamu, kumeza chungu
KAMPENI za uchaguzi mdogo katika jimbo la Igunga, mkoani Tabora zinatarajiwa kuanza mjini humo Alhamisi wiki hii. Tayari viroja vya wanasiasa vimeanza na anayetegemea kuona au kusikia matumizi ya akili huko Igunga anajisumbua. Huu utakuwa mwezi wa kupumzisha akili na ukweli, kisha kutumia unafiki na uwongo ili kunogesha siasa za nchi yetu.
Kwa hali ilivyo ni mchuano kati ya CHADEMA na vyama vingine.
CHADEMA wametoa somo, lizingatiwe
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewafuta uanachama madiwani wake watano wa mkoa wa Arusha. Wengine wanasema haya ndiyo maamuzi magumu.

Mchungaji Msigwa: Tuna viongozi legelege
HANA makeke. Ni mpole, lakini mwenye msimamo thabiti wa kutetea anachokiamini. Si mwingine, bali Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Bunge la Muungano katika jimbo la Iringa Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Taa ya njano yaiwakia CHADEMA
RANGI ya njano imetumika mahali pengi kama alama ya tahadhari. Wanaoendesha vyombo vya moto kama vile magari na pikipiki wanajua kwamba taa ya njano ikiwaka inamtahadharisha dereva kujiandaa kuchukua uamuzi; kusimama au kuendelea kuendesha.

CCM karibu ife: Vijana wafuate nini huko?
GAZETI la Citizen la 20 Aprili 2011, lilichapisha makala ya Ayub Rioba, ikimsifu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilson Mukama, kwamba ni mtu mwenye uwezo wa kukifufua chama hicho.
Unafiki wa CHADEMA, ulafi wa CCM
TAKRIBANI majuma mawili sasa, Bunge la Jamhuri na baadhi ya vyombo vya habari nchini vimetawaliwa na mjadala wa posho za wabunge na watumishi wa serikali.

Spika Makinda, kazi kwako!
FEBRUARI 6, 2008, Spika wa Bunge la 9 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyekuwa Spika wa Bunge, Samweli Sitta alitoa dokezo zito kuhusu naibu wake Anne Makinda.

Mbunge: Katiba imevunjwa
HOJA ya Rais Jakaya Kikwete kusaini Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011-2016) kabla bunge kuujadili, imeibua shutuma kwa ofisi kuu nchini.

CCM wapanga kuhujumu CHADEMA
MKAKATI wa makusudi umesukwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kudhoofisha jitihada za kisiasa za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), MwanaHALISI limeelezwa.

Ukombozi waja… kipigo chayoyoma
NJIA bora ya kuharakisha mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini Tanzania ni kubughudhi viongozi wa upinzani kila kukicha.

Matatizo mengine CHADEMA mnajitakia
UCHAGUZI mkuu wa kuchagua viongozi wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA) umekuja na mambo yake. Mengine yalitarajiwa na mengine hayakutarajiwa.
NEC na uparaganyaji siasa KigomaUjiji
JIMBO la Uchaguzi la Kigoma Mjini limekuwa na upinzani mkubwa kisiasa unaohusisha vyama vya CCM na CHADEMA kwa kipindi chote tangu mfumo wa vyama vingi uliporudishwa mwaka 1992.

Maandamano haya yaungwe mkono
NIMEFUATILIA kwa muda maandamano yanayofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) toka mwanzo wake na nimejaribu kutumia muda kuyaelewa. Mwanzoni niliyaona kama maandamano ya watu ambao bado wana machungu ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa 30 Oktoba 2010.

Benson: CCM incheza ngoma ya CHADEMA
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakikushinda uchaguzi mkuu mwaka 2010 kiliangushwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katiba Mpya: Tunachotaka sasa
KUNA madai kwamba kinachohitajika sasa ni kuwaelimisha wananchi juu ya katiba iliyopo kabla ya kuandika katika mpya. Nina maoni tofauti.

Mjadala wa Katiba kama usanii
ENEO la Karimjee, ukumbi maarufu jijini Dar es Salaam. Nakuta mjadala wa muswada wa sheria ya marejeo/mapitio ya Katiba wa 2011 ndio kwanza umeanza.
Uislam wa CCM na Ukiristo wa CHADEMA
NALAZIMIKA kuandika makala hii ili kutoa mchango wangu juu ya mjadala tete unaoendelezwa na viongozi wa dini na wanasiasa. Kwa kuwa imekuwa kawaida kwa watu kuzungumzia suala hili jumlajumla tu.

Prof. Safari: Saa ya ukombozi ni sasa
UAMUZI wa mwanaharakati maarufu wa haki za waislamu, Profesa Abdallah Jumbe Safari (59) kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), umetikisa siasa za Tanzania.

DIWANI YUSUPH: Napigania elimu, afya na ulinzi
KUTANA na Yusuph Fungameza (44), diwani wa kata ya Uyovu, wilaya ya Bukombe mkoani Shinyanga.

CUF, NCCR wajipakaza uoza wa CCM
KAMA viongozi wa NCCR-Mageuzi, Chama cha Wananchi (CUF), Tanzania Labour Party (TLP) na United Democratic Party (UDP) wangekaa chini na kupima sababu za kuporomoka kisiasa kwa Mchungaji Christopher Mtikila wa DP, wasingekubali mwaliko wa ikulu kunywa sifongo.

Rais mtarajiwa ni mzushi
MIONGONI mwa watu wanaotajwa kuwa kwenye mzunguko wa mwisho kuelekea ikulu katika uchaguzi mkuu ujao ni Bernard Kamilius Membe.

Membe asilishe watu siasa chafu
MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na Bernard Membe, wametoa tuhuma nzito kuhusu ustawi wa siasa nchini. Kwa nyakati tofauti, Membe na Simba wametuhumu mataifa ya nje kuwa yanajiingiza katika siasa za ndani ya nchi kwa kufadhili chama kimoja cha siasa ili kifanye vurugu na kuvunja amani ambayo imetamalaki nchini kwa miaka mingi.

CCM na kisa cha King Oedipus
BAADHI wanaweza kuwa wamesoma kitabu cha King Oedipus (The Sophocles) katika saikolojia na wengine katika fasihi. Kisa hicho, ni mfano mzuri kwa watu wanaohaha kukwepa janga, lakini wakashindwa kuzuia janga hilo kutokea.

Sumaye kasema kweli: CCM wajibu hoja za kisiasa
WAZIRI mkuu mstaafu, Fredick Sumaye amekirejesha darasani chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM). Sumaye anaamini CCM hakijahitimu au kimepotea njia. Anataka kisome upya ili hatimaye kiweze kutunukiwa cheti cha ushindani katika mfumo wa vyama vingi.
Steven Wassira anatumikia mtandao, si serikali
STEVEN Wassira ni waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu katika jamii. Yasemekana lengo kuu la wizara hii ni kushughulikia mahusiano katika jamii na kuhakikisha migogoro inadhibitiwa kabla haijatokea.