CHADEMA


Mlolongo wa Habari za Chama cha Demokrasia na Maendeleo

Mwandishi wetu's picture

Regia alifanya mengi makubwa


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 18 January 2012

REGIA Estelatus Mtema hatunaye; ametutoka ghafla na kuacha majonzi. Ajali mbaya aliyopata saa 5.30 hivi Jumamosi iliyopita eneo la Ruvu mkoani Pwani ndiyo imepora maisha yake. Anatarajiwa kuzikwa kwao Ifakara, Kilombero.

Wazazi wanalia, ndugu na jamaa wanalia; waliokua, kusoma, kufanya kazi naye wanasikitika. Wanasiasa hasa wanachama, wafuasi na viongozi wa chama chake – Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wanaombeleza kumpoteza mbunge huyo kijana na mpambanaji.

Alfred Lucas's picture

Opulukwa: Nipo vitani Meatu, nitashinda


Na Alfred Lucas - Imechapwa 21 December 2011

MBUNGE wa jimbo la Meatu, Meshack Opulukwa anapiga mayowe. Kwa miezi miwili hakuna anayemsikiliza. Amekuwa akihangaika kutafuta ufumbuzi baada ya serikali ya mkoa kuamuru operesheni ya kuhamisha kwa nguvu makazi ya watu katika kijiji cha Mwangudo, ndani ya jimbo analoliwakilisha.

Uhamishaji huo umefanywa kwa sababu ya kinachoelezwa wananchi “wanaishi ndani ya hifadhi ya jamii ya Makao.” Matokeo ya operesheni hiyo ni kuteketezwa kwa moto zaidi ya nyumba 1,000 za wananchi na mamia ya watu kuumia.

Saed Kubenea's picture

Kikwete akaliwa kooni


Na Saed Kubenea - Imechapwa 14 December 2011

Naye atakiwa kujiuzulu
Waraka mzito wavuja
CHADEMA yaitwa ‘mchawi’

RAIS Jakaya Kikwete amekaliwa kooni. Wakati chama chake kinakabiliwa na wimbi la kukimbiwa na wanachama na viongozi, swahiba wake anashikilia kuwa wenye “tuhuma za ufisadi” wajiuzulu kama yeye.

Alfred Lucas's picture

Waziri kumkimbia Lowassa CCM


Na Alfred Lucas - Imechapwa 07 December 2011

WAZIRI mmoja mwandamizi ndani ya serikali ya Rais Jakaya Kikwete, yuko mbioni kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM), imefahamika.

Fred Okoth's picture

CHADEMA yatikisa Ikulu


Na Fred Okoth - Imechapwa 30 November 2011

RAIS Jakaya Kikwete hakufahamu kwa undani kilichomo kwenye muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba (Constitutional Review Bill 2011), uliopitishwa na bunge hivi karibuni, MwanaHALISI limeelezwa.

mashinda's picture

CCM: Kutema tamu, kumeza chungu


Na mashinda - Imechapwa 12 September 2011

KAMPENI za uchaguzi mdogo katika jimbo la Igunga, mkoani Tabora zinatarajiwa kuanza mjini humo Alhamisi wiki hii. Tayari viroja vya wanasiasa vimeanza na anayetegemea kuona au kusikia matumizi ya akili huko Igunga anajisumbua. Huu utakuwa mwezi wa kupumzisha akili na ukweli, kisha kutumia unafiki na uwongo ili kunogesha siasa za nchi yetu.

Kwa hali ilivyo ni mchuano kati ya CHADEMA na vyama vingine.

Paschally Mayega's picture

CHADEMA wametoa somo, lizingatiwe


Na Paschally Mayega - Imechapwa 17 August 2011

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewafuta uanachama madiwani wake watano wa mkoa wa Arusha. Wengine wanasema haya ndiyo maamuzi magumu.

Mwandishi wetu's picture

Mchungaji Msigwa: Tuna viongozi legelege


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 27 July 2011

HANA makeke. Ni mpole, lakini mwenye msimamo thabiti wa kutetea anachokiamini. Si mwingine, bali Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Bunge la Muungano katika jimbo la Iringa Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Paschally Mayega's picture

Taa ya njano yaiwakia CHADEMA


Na Paschally Mayega - Imechapwa 06 July 2011

RANGI ya njano imetumika mahali pengi kama alama ya tahadhari. Wanaoendesha vyombo vya moto kama vile magari na pikipiki wanajua kwamba taa ya njano ikiwaka inamtahadharisha dereva kujiandaa kuchukua uamuzi; kusimama au kuendelea kuendesha.

Mabere Marando's picture

CCM karibu ife: Vijana wafuate nini huko?


Na Mabere Marando - Imechapwa 06 July 2011

GAZETI la Citizen la 20 Aprili 2011, lilichapisha makala ya Ayub Rioba, ikimsifu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilson Mukama, kwamba ni mtu mwenye uwezo wa kukifufua chama hicho.

Kondo Tutindaga's picture

Unafiki wa CHADEMA, ulafi wa CCM


Na Kondo Tutindaga - Imechapwa 29 June 2011

TAKRIBANI majuma mawili sasa, Bunge la Jamhuri na baadhi ya vyombo vya habari nchini vimetawaliwa na mjadala wa posho za wabunge na watumishi wa serikali.

Joster Mwangulumbi's picture

Spika Makinda, kazi kwako!


Na Joster Mwangulumbi - Imechapwa 29 June 2011

FEBRUARI 6, 2008, Spika wa Bunge la 9 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyekuwa Spika wa Bunge, Samweli Sitta alitoa dokezo zito kuhusu naibu wake Anne Makinda.

Mwandishi Maalum's picture

Mbunge: Katiba imevunjwa


Na Mwandishi Maalum - Imechapwa 15 June 2011

HOJA ya Rais Jakaya Kikwete kusaini Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011-2016) kabla bunge kuujadili, imeibua shutuma kwa ofisi kuu nchini.

Alfred Lucas's picture

CCM wapanga kuhujumu CHADEMA


Na Alfred Lucas - Imechapwa 08 June 2011

MKAKATI wa makusudi umesukwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kudhoofisha jitihada za kisiasa za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), MwanaHALISI limeelezwa.

Ndimara Tegambwage's picture

Ukombozi waja… kipigo chayoyoma


Na Ndimara Tegambwage - Imechapwa 08 June 2011

NJIA bora ya kuharakisha mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini Tanzania ni kubughudhi viongozi wa upinzani kila kukicha.

M. M. Mwanakijiji's picture

Matatizo mengine CHADEMA mnajitakia


Na M. M. Mwanakijiji - Imechapwa 01 June 2011

UCHAGUZI mkuu wa kuchagua viongozi wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA) umekuja na mambo yake. Mengine yalitarajiwa na mengine hayakutarajiwa.

Anthony Kayanda's picture

NEC na uparaganyaji siasa KigomaUjiji


Na Anthony Kayanda - Imechapwa 01 June 2011

JIMBO la Uchaguzi la Kigoma Mjini limekuwa na upinzani mkubwa kisiasa unaohusisha vyama vya CCM na CHADEMA kwa kipindi chote tangu mfumo wa vyama vingi uliporudishwa mwaka 1992.

M. M. Mwanakijiji's picture

Maandamano haya yaungwe mkono


Na M. M. Mwanakijiji - Imechapwa 11 May 2011

NIMEFUATILIA kwa muda maandamano yanayofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) toka mwanzo wake na nimejaribu kutumia muda kuyaelewa. Mwanzoni niliyaona kama maandamano ya watu ambao bado wana machungu ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa 30 Oktoba 2010.

Alfred Lucas's picture

Benson: CCM incheza ngoma ya CHADEMA


Na Alfred Lucas - Imechapwa 27 April 2011

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakikushinda uchaguzi mkuu mwaka 2010 kiliangushwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mabere Marando's picture

Katiba Mpya: Tunachotaka sasa


Na Mabere Marando - Imechapwa 20 April 2011

KUNA madai kwamba kinachohitajika sasa ni kuwaelimisha wananchi juu ya katiba iliyopo kabla ya kuandika katika mpya. Nina maoni tofauti.

Mwandishi wetu's picture

Mjadala wa Katiba kama usanii


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 13 April 2011

ENEO la Karimjee, ukumbi maarufu jijini Dar es Salaam. Nakuta mjadala wa muswada wa sheria ya marejeo/mapitio ya Katiba wa 2011 ndio kwanza umeanza.

Kondo Tutindaga's picture

Uislam wa CCM na Ukiristo wa CHADEMA


Na Kondo Tutindaga - Imechapwa 06 April 2011

NALAZIMIKA kuandika makala hii ili kutoa mchango wangu juu ya mjadala tete unaoendelezwa na viongozi wa dini na wanasiasa. Kwa kuwa imekuwa kawaida kwa watu kuzungumzia suala hili jumlajumla tu.

Ezekiel Kamwaga's picture

Prof. Safari: Saa ya ukombozi ni sasa


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 06 April 2011

UAMUZI wa mwanaharakati maarufu wa haki za waislamu,  Profesa Abdallah Jumbe Safari (59) kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), umetikisa siasa za Tanzania.

Yusuf Aboud's picture

DIWANI YUSUPH: Napigania elimu, afya na ulinzi


Na Yusuf Aboud - Imechapwa 23 March 2011

KUTANA na Yusuph Fungameza (44), diwani wa kata ya Uyovu, wilaya ya Bukombe mkoani Shinyanga.

Mwandishi wetu's picture

CUF, NCCR wajipakaza uoza wa CCM


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 23 March 2011

KAMA viongozi wa NCCR-Mageuzi, Chama cha Wananchi (CUF), Tanzania Labour Party (TLP) na United Democratic Party (UDP) wangekaa chini na kupima sababu za kuporomoka kisiasa kwa Mchungaji Christopher Mtikila wa DP, wasingekubali mwaliko wa ikulu kunywa sifongo.

Joster Mwangulumbi's picture

Rais mtarajiwa ni mzushi


Na Joster Mwangulumbi - Imechapwa 16 March 2011

MIONGONI mwa watu wanaotajwa kuwa kwenye mzunguko wa mwisho kuelekea ikulu katika uchaguzi mkuu ujao ni Bernard Kamilius Membe.

Isaac Kimweri's picture

Membe asilishe watu siasa chafu


Na Isaac Kimweri - Imechapwa 16 March 2011

MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na Bernard Membe, wametoa tuhuma nzito kuhusu ustawi wa siasa nchini. Kwa nyakati tofauti, Membe na Simba wametuhumu mataifa ya nje kuwa yanajiingiza katika siasa za ndani ya nchi kwa kufadhili chama kimoja cha siasa ili kifanye vurugu na kuvunja amani ambayo imetamalaki nchini kwa miaka mingi.

Joster Mwangulumbi's picture

CCM na kisa cha King Oedipus


Na Joster Mwangulumbi - Imechapwa 09 March 2011

BAADHI wanaweza kuwa wamesoma kitabu cha King Oedipus (The Sophocles) katika saikolojia na wengine katika fasihi. Kisa hicho, ni mfano mzuri kwa watu wanaohaha kukwepa janga, lakini wakashindwa kuzuia janga hilo kutokea.

Saed Kubenea's picture

Sumaye kasema kweli: CCM wajibu hoja za kisiasa


Na Saed Kubenea - Imechapwa 09 March 2011

WAZIRI mkuu mstaafu, Fredick Sumaye amekirejesha darasani chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM). Sumaye anaamini CCM hakijahitimu au kimepotea njia. Anataka kisome upya ili hatimaye kiweze kutunukiwa cheti cha ushindani katika mfumo wa vyama vingi.

Kondo Tutindaga's picture

Steven Wassira anatumikia mtandao, si serikali


Na Kondo Tutindaga - Imechapwa 09 March 2011

STEVEN Wassira ni waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano  na Uratibu katika jamii. Yasemekana lengo kuu la wizara hii ni kushughulikia mahusiano katika jamii na kuhakikisha migogoro inadhibitiwa kabla haijatokea.