CUF


Mlolongo wa Habari za Chama cha Wananchi

Jabir Idrissa's picture

Urais Zanzibar waitafuna CUF


Na Jabir Idrissa - Imechapwa 04 January 2012

MGOGORO unaofukuta kati ya katibu mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad na mbunge wa Wawi, kisiwani Pemba, Hamad Rashid Mohamed, chimbuko lake, ni mbio za urais wa Zanzibar mwaka 2015, imefahamika.

Saed Kubenea's picture

Mpango wa CCM ‘kuua’ CUF waelekea kufanikiwa


Na Saed Kubenea - Imechapwa 04 January 2012

KIKAO cha dharura cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama cha Wananchi (CUF), kimeitishwa mjini Zanzibar leo (4 Junuari 2012) ili kubariki “mradi” wa kumvua uanachama mbunge wa Wawi kisiwani Pemba, Hamad Rashid Mohammed.

Saed Kubenea's picture

Hamad kufukuzwa CUF


Na Saed Kubenea - Imechapwa 28 December 2011

ALIYEJIAPIZA kumng’oa Maalim Seif Shariff Hamad ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), sasa kufukuzwa uanachama, imefahamika.

Jabir Idrissa's picture

CUF inao au haina mgogoro?


Na Jabir Idrissa - Imechapwa 28 December 2011

“CHAMA chetu hakina mgogoro,” anasema Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad, katika kuelezea mvutano ulioibuka ndani ya chama hicho.

Maalim Seif, mmoja wa wanasiasa wa enzi nchini walioanzisha CUF mwaka 1992, anasema kwa kuwa chama ambacho yeye ni kiongozi mtendaji mkuu, hakina mgogoro wowote, anatarajia kama lipo tatizo linalokihusu lipite kwenye vikao halali.

Kwa sababu yale yanayohojiwa hayajapita kwenye vikao, anasema “kamwe sithubutu kuendesha malumbano na mtu yeyote.

Alfred Lucas's picture

Ufa wazidi kuongezeka CUF


Na Alfred Lucas - Imechapwa 14 December 2011

UFA ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), umezidi kuongezeka. Wakati idara ya usalama ya chama hicho ikisema Hamad Rashid Mohammed, anatumiwa na Edward Lowassa katika mbio zake za kutafuta uongozi, Maalim Seif Shariff Hamad, anasema yeye mwenyewe ndiye anayesaka urais.

Mbasha Asenga's picture

Kuna mtihani wa kuua siasa feki


Na Mbasha Asenga - Imechapwa 07 December 2011

DUNIANI sasa kuna vita dhidi ya bidhaa bandia (feki). Hapa nchini Tume ya Ushindani wa Biashara (FCC) imekuwa na jukumu la kuteketeza bidhaa feki kwa kushirikiana na Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Bidhaa feki ni uhalifu. Ni kutengeneza bidhaa inayofanana na nyingine, kwa nia moja tu, kujipata faida kubwa kwa kuigiza kitu ambacho kina jina kubwa na hivyo kulaghai wateja kuwa inawauzia kitu halisi kumbe ni feki.

Mambo ya kuigiza hayapo kwenye bidhaa tu. Wapo watu wa aina kwa aina ambao huiga wengine kila siku iendayo kwa Mola.

Mwandishi Maalum's picture

CUF na kiherehere cha ikulu


Na Mwandishi Maalum - Imechapwa 07 December 2011

NIMEJITOSA kujadili hatua ya viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) kujipeleka ikulu kuonana na Rais Jakaya Kikwete. Kwangu mimi hatua ile ya CUF naiona kama ni kujikanyaga.

Alfred Lucas's picture

Mahona: Natembea na ushindi Igunga


Na Alfred Lucas - Imechapwa 31 August 2011

LEOPOLD Lucas Mahona, mwanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) aliyepitishwa kuwania ubunge Jimbo la Igunga amesema tayari ana mtaji wa ushindi kutokana na kura alizopata katika uchaguzi mkuu mwaka jana.

Jabir Idrissa's picture

CCM, CUF serikalini ‘tuko makini’


Na Jabir Idrissa - Imechapwa 29 June 2011

MIEZI saba baada ya kuundwa kwa serikali iliyoshirikisha vyama viwili vilivyokuwa hasimu kisiasa visiwani Zanzibar – Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar imethibitisha kuwa hakuna kisichowezekana.

Ezekiel Kamwaga's picture

Kadhia ya Sakaya na bao la kujifunga la CUF


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 29 June 2011

MAGDALENA Sakaya, mbunge wa Viti Maalumu kupitia Chama cha Wananchi (CUF) na viongozi wengine wa juu wa chama hicho, walikaa rumande ya polisi kwa muda wa siku mbili.

Ezekiel Kamwaga's picture

Sakaya: Tumetendewa unyama Urambo


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 22 June 2011

MAGDALENA Sakaya, Mbunge wa Viti Maalumu (CUF) kutoka mkoa wa Tabora ameonja kadhia kubwa katika harakati za kuwasaidia wananchi wake kupata ufumbuzi wa matatizo yanayowakabili.

Ezekiel Kamwaga's picture

Kadhia ya Magdalena Sakaya


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 22 June 2011

KUANZIA Mei 28 hadi Juni 7 mwaka huu, Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tabora (CUF), Magdalena Sakaya, alishikiliwa katika mahabusu ya gereza la wanawake wilayani Urambo mkoani Tabora.

Saed Kubenea's picture

CUF inavyozama huku ikidhoofisha upinzani


Na Saed Kubenea - Imechapwa 08 June 2011

CHAMA cha Wananchi (CUF) chaweza sasa kuwa kinatoka usingizini? Lakini wapo wanaosema, “Kinatafuta shuka wakati tayari kumekucha.”

Jabir Idrissa's picture

NCCR ipi ya kushikamana na CUF leo?


Na Jabir Idrissa - Imechapwa 06 April 2011

TAZAMA picha hii: Profesa Ibrahim Lipumba na James Mbatia wamesimama pamoja jukwaani. Mikono yao miwili imeshikamana. Profesa ndiye ameshika mkono wa kushoto wa Mbatia kwa kutumia mkono wake wa kulia. Ameuinua juu na anapiga mayowe ya mshikamano.

Jabir Idrissa's picture

Kumbe kustaafu ni mchezo wa kuigiza tu


Na Jabir Idrissa - Imechapwa 23 February 2011

YUSSUF Omar Chunda, mtangazaji wa zamani wa redio, anakumbuka alivyoandaliwa sherehe nzito na wafanyakazi wa Sauti ya Tanzania Zanzibar (STZ) alipostaafu utumishi wa serikali mwishoni mwa mwaka jana.

Ezekiel Kamwaga's picture

Buriani Mazee Rajab Mazee


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 16 February 2011

ASUBUHI ya Jumapili iliyopita ilikuwa mbaya kwangu. Majira ya saa 1: 14, nilipokea ujumbe mfupi wa maneno kwa njia ya simu kutoka kwa Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro.

Saed Kubenea's picture

Hujuma dhidi ya CHADEMA nje


Na Saed Kubenea - Imechapwa 02 February 2011

Zitto kung’olewa rasmi

MRADI wa vyama vitatu vya upinzani nchini unaolenga kupunguza nguvu za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bungeni, huenda ukakwama.

Yusuf Aboud's picture

Mbalamwezi: Prof Lipumba aache uenyekiti


Na Yusuf Aboud - Imechapwa 02 February 2011

OMAR Said Mbalamwezi amechoka na amekata tamaa kisiasa. Anaona Chama cha Wananchi (CUF) alichojiunga tangu kilipoanzishwa mwaka 1992, kinaelekea kubaya.

Mbasha Asenga's picture

Hamad Rashid anatamani kuwa popo


Na Mbasha Asenga - Imechapwa 25 January 2011

KWA siku mbili mfululizo niliwasha kompyuta yangu niandike hiki nitakachoandika leo, lakini nikawa nasita na kujizuia kufanya hivyo.

Ezekiel Kamwaga's picture

Anenayo leo Profesa Abdallah Safari


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 25 January 2011

PROFESA Abdallah Jumbe Safari ni mtu wa vipaji vingi. Ni mwanasheria aliyebobea. Ni mtaalamu wa lugha ya Kiswahili na mtunzi wa vitabu vya riwaya na vya taaluma yake.

Ezekiel Kamwaga's picture

Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 25 January 2011

KAULI aliyoitoa Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro kuhusu uanachama wa Profesa Abdallah Safari ina madhara.

Ezekiel Kamwaga's picture

Mtatiro: Nitarejesha makali ya CUF


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 22 December 2010

MIONGONI mwa wanasiasa vijana waliopo nchini kwa sasa, Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro, ana historia ya kipekee.

Yusuf Aboud's picture

CHADEMA, CUF: Mpinzani atajulikana kesho


Na Yusuf Aboud - Imechapwa 01 December 2010

NIMEMSIKILIZA vema Hamad Rashid Mohammed, Mbunge wa Wawi, akizungumza katika mdahalo wa wazi ulioandaliwa na Vox Media na East Africa Business and Media Training Institute (EABMTI), kwa ufadhili wa ITV, mwishoni mwa wiki.

Hilal K. Sued's picture

CUF wapoteza mwelekeo wa upinzani


Na Hilal K. Sued - Imechapwa 01 December 2010

UPINZANI ni kitu cha msaada mkubwa sana katika siasa na maendeleo ya demokrasia ya nchi. Lakini katika nchi nyingi hii imebaki nadharia tu, katika uhalisia upinzani unaonekana kuwa ni uadui mkubwa dhidi ya chama tawala.

Saed Kubenea's picture

CUF yajiandaa kuvuruga upinzani bungeni?


Na Saed Kubenea - Imechapwa 24 November 2010

CHAMA cha Wananchi (CUF) kinaonekana kupumbazwa na “ndoa ya mkeka” kiliyofunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM)?

Jabir Idrissa's picture

Mawaziri sawa, makatibu wakuu hapana


Na Jabir Idrissa - Imechapwa 24 November 2010

WAKATI ukuta, ukipambana nao utaumia. Uteuzi wa mawaziri alioufanya Rais Dk. Ali Mohamed Shein umejumuisha mawaziri wanane kutoka Chama cha Wananchi (CUF) kuingia katika Baraza la Mapinduzi (BLM), nguzo kubwa ya kuendeleza misingi ya mapinduzi ya 12 Januari 1964.

Ezekiel Kamwaga's picture

Prof Lipumba: ‘Rais’ bora anyekosa kura za kutosha


Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 17 November 2010

WIKI iliyopita nilieleza kwa ujumla sifa za aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ikilinganishwa na waliokuwa wapinzani wake katika uchaguzi uliopita.

Mwandishi wetu's picture

Baruany: Kiboko cha Abdulaziz


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 10 November 2010

SALUM Khafan Nassor Baruany (51), mbunge mteule wa Jimbo la Lindi Mjini, ameweka historia ya kuwa mtu wa kwanza nchini mwenye ulemavu wa ngozi (albino) kushika wadhifa huo kupitia njia ya kuchaguliwa na wananchi.

Mwandishi wetu's picture

Maalim Seif amezaliwa upya


Na Mwandishi wetu - Imechapwa 03 November 2010

BAADA ya matukio yaliyotokea Zanzibar katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, ni wazi jina la Maalim Seif Shariff Hamad, litabaki katika vitabu vya historia ya visiwa hivyo kwa miaka mingi ijayo.

Joster Mwangulumbi's picture

Fatma Maghimbi ajiziba mdomo


Na Joster Mwangulumbi - Imechapwa 27 October 2010

WANASIASA wengi ni kama samaki aina ya mkizi. Wana hasira ambazo mara nyingine huwaponza na ndiyo kiini cha methali isemayo “ana hasira za mkizi.”