CUF
Mlolongo wa Habari za Chama cha Wananchi

Urais Zanzibar waitafuna CUF
MGOGORO unaofukuta kati ya katibu mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad na mbunge wa Wawi, kisiwani Pemba, Hamad Rashid Mohamed, chimbuko lake, ni mbio za urais wa Zanzibar mwaka 2015, imefahamika.

Mpango wa CCM ‘kuua’ CUF waelekea kufanikiwa
KIKAO cha dharura cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama cha Wananchi (CUF), kimeitishwa mjini Zanzibar leo (4 Junuari 2012) ili kubariki “mradi” wa kumvua uanachama mbunge wa Wawi kisiwani Pemba, Hamad Rashid Mohammed.

Hamad kufukuzwa CUF
ALIYEJIAPIZA kumng’oa Maalim Seif Shariff Hamad ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), sasa kufukuzwa uanachama, imefahamika.

CUF inao au haina mgogoro?
“CHAMA chetu hakina mgogoro,” anasema Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad, katika kuelezea mvutano ulioibuka ndani ya chama hicho.
Maalim Seif, mmoja wa wanasiasa wa enzi nchini walioanzisha CUF mwaka 1992, anasema kwa kuwa chama ambacho yeye ni kiongozi mtendaji mkuu, hakina mgogoro wowote, anatarajia kama lipo tatizo linalokihusu lipite kwenye vikao halali.
Kwa sababu yale yanayohojiwa hayajapita kwenye vikao, anasema “kamwe sithubutu kuendesha malumbano na mtu yeyote.

Ufa wazidi kuongezeka CUF
UFA ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), umezidi kuongezeka. Wakati idara ya usalama ya chama hicho ikisema Hamad Rashid Mohammed, anatumiwa na Edward Lowassa katika mbio zake za kutafuta uongozi, Maalim Seif Shariff Hamad, anasema yeye mwenyewe ndiye anayesaka urais.

Kuna mtihani wa kuua siasa feki
DUNIANI sasa kuna vita dhidi ya bidhaa bandia (feki). Hapa nchini Tume ya Ushindani wa Biashara (FCC) imekuwa na jukumu la kuteketeza bidhaa feki kwa kushirikiana na Shirika la Viwango Tanzania (TBS).
Bidhaa feki ni uhalifu. Ni kutengeneza bidhaa inayofanana na nyingine, kwa nia moja tu, kujipata faida kubwa kwa kuigiza kitu ambacho kina jina kubwa na hivyo kulaghai wateja kuwa inawauzia kitu halisi kumbe ni feki.
Mambo ya kuigiza hayapo kwenye bidhaa tu. Wapo watu wa aina kwa aina ambao huiga wengine kila siku iendayo kwa Mola.

CUF na kiherehere cha ikulu
NIMEJITOSA kujadili hatua ya viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) kujipeleka ikulu kuonana na Rais Jakaya Kikwete. Kwangu mimi hatua ile ya CUF naiona kama ni kujikanyaga.

Mahona: Natembea na ushindi Igunga
LEOPOLD Lucas Mahona, mwanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) aliyepitishwa kuwania ubunge Jimbo la Igunga amesema tayari ana mtaji wa ushindi kutokana na kura alizopata katika uchaguzi mkuu mwaka jana.

CCM, CUF serikalini ‘tuko makini’
MIEZI saba baada ya kuundwa kwa serikali iliyoshirikisha vyama viwili vilivyokuwa hasimu kisiasa visiwani Zanzibar – Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar imethibitisha kuwa hakuna kisichowezekana.

Kadhia ya Sakaya na bao la kujifunga la CUF
MAGDALENA Sakaya, mbunge wa Viti Maalumu kupitia Chama cha Wananchi (CUF) na viongozi wengine wa juu wa chama hicho, walikaa rumande ya polisi kwa muda wa siku mbili.

Sakaya: Tumetendewa unyama Urambo
MAGDALENA Sakaya, Mbunge wa Viti Maalumu (CUF) kutoka mkoa wa Tabora ameonja kadhia kubwa katika harakati za kuwasaidia wananchi wake kupata ufumbuzi wa matatizo yanayowakabili.

Kadhia ya Magdalena Sakaya
KUANZIA Mei 28 hadi Juni 7 mwaka huu, Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tabora (CUF), Magdalena Sakaya, alishikiliwa katika mahabusu ya gereza la wanawake wilayani Urambo mkoani Tabora.

CUF inavyozama huku ikidhoofisha upinzani
CHAMA cha Wananchi (CUF) chaweza sasa kuwa kinatoka usingizini? Lakini wapo wanaosema, “Kinatafuta shuka wakati tayari kumekucha.”

NCCR ipi ya kushikamana na CUF leo?
TAZAMA picha hii: Profesa Ibrahim Lipumba na James Mbatia wamesimama pamoja jukwaani. Mikono yao miwili imeshikamana. Profesa ndiye ameshika mkono wa kushoto wa Mbatia kwa kutumia mkono wake wa kulia. Ameuinua juu na anapiga mayowe ya mshikamano.

Kumbe kustaafu ni mchezo wa kuigiza tu
YUSSUF Omar Chunda, mtangazaji wa zamani wa redio, anakumbuka alivyoandaliwa sherehe nzito na wafanyakazi wa Sauti ya Tanzania Zanzibar (STZ) alipostaafu utumishi wa serikali mwishoni mwa mwaka jana.

Buriani Mazee Rajab Mazee
ASUBUHI ya Jumapili iliyopita ilikuwa mbaya kwangu. Majira ya saa 1: 14, nilipokea ujumbe mfupi wa maneno kwa njia ya simu kutoka kwa Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro.

Hujuma dhidi ya CHADEMA nje
- Zitto kung’olewa rasmi
MRADI wa vyama vitatu vya upinzani nchini unaolenga kupunguza nguvu za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bungeni, huenda ukakwama.

Mbalamwezi: Prof Lipumba aache uenyekiti
OMAR Said Mbalamwezi amechoka na amekata tamaa kisiasa. Anaona Chama cha Wananchi (CUF) alichojiunga tangu kilipoanzishwa mwaka 1992, kinaelekea kubaya.

Hamad Rashid anatamani kuwa popo
KWA siku mbili mfululizo niliwasha kompyuta yangu niandike hiki nitakachoandika leo, lakini nikawa nasita na kujizuia kufanya hivyo.

Anenayo leo Profesa Abdallah Safari
PROFESA Abdallah Jumbe Safari ni mtu wa vipaji vingi. Ni mwanasheria aliyebobea. Ni mtaalamu wa lugha ya Kiswahili na mtunzi wa vitabu vya riwaya na vya taaluma yake.

Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni
KAULI aliyoitoa Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro kuhusu uanachama wa Profesa Abdallah Safari ina madhara.

Mtatiro: Nitarejesha makali ya CUF
MIONGONI mwa wanasiasa vijana waliopo nchini kwa sasa, Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro, ana historia ya kipekee.

CHADEMA, CUF: Mpinzani atajulikana kesho
NIMEMSIKILIZA vema Hamad Rashid Mohammed, Mbunge wa Wawi, akizungumza katika mdahalo wa wazi ulioandaliwa na Vox Media na East Africa Business and Media Training Institute (EABMTI), kwa ufadhili wa ITV, mwishoni mwa wiki.
CUF wapoteza mwelekeo wa upinzani
UPINZANI ni kitu cha msaada mkubwa sana katika siasa na maendeleo ya demokrasia ya nchi. Lakini katika nchi nyingi hii imebaki nadharia tu, katika uhalisia upinzani unaonekana kuwa ni uadui mkubwa dhidi ya chama tawala.

CUF yajiandaa kuvuruga upinzani bungeni?
CHAMA cha Wananchi (CUF) kinaonekana kupumbazwa na “ndoa ya mkeka” kiliyofunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM)?

Mawaziri sawa, makatibu wakuu hapana
WAKATI ukuta, ukipambana nao utaumia. Uteuzi wa mawaziri alioufanya Rais Dk. Ali Mohamed Shein umejumuisha mawaziri wanane kutoka Chama cha Wananchi (CUF) kuingia katika Baraza la Mapinduzi (BLM), nguzo kubwa ya kuendeleza misingi ya mapinduzi ya 12 Januari 1964.

Prof Lipumba: ‘Rais’ bora anyekosa kura za kutosha
WIKI iliyopita nilieleza kwa ujumla sifa za aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ikilinganishwa na waliokuwa wapinzani wake katika uchaguzi uliopita.

Baruany: Kiboko cha Abdulaziz
SALUM Khafan Nassor Baruany (51), mbunge mteule wa Jimbo la Lindi Mjini, ameweka historia ya kuwa mtu wa kwanza nchini mwenye ulemavu wa ngozi (albino) kushika wadhifa huo kupitia njia ya kuchaguliwa na wananchi.

Maalim Seif amezaliwa upya
BAADA ya matukio yaliyotokea Zanzibar katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, ni wazi jina la Maalim Seif Shariff Hamad, litabaki katika vitabu vya historia ya visiwa hivyo kwa miaka mingi ijayo.

Fatma Maghimbi ajiziba mdomo
WANASIASA wengi ni kama samaki aina ya mkizi. Wana hasira ambazo mara nyingine huwaponza na ndiyo kiini cha methali isemayo “ana hasira za mkizi.”