Dowans
Mlolongo wa Habari za kashfa ya Dowans

Lowassa anajua uzalendo au ni ‘machozi ya mamba?’
EDWARD Lowassa, yule aliyejiuzulu nafasi ya waziri mkuu kutokana na kashifa ya kuingiza nchi kwenye mkataba wa kinyonyaji wa makampuni ya Richmond/Dowans, sasa anasaka utakaso.

Symbion: Mwanzo au mwisho wa kashfa?
SERIKALI ya Rais Jakaya Kikwete iliridhia mapendekezo ya Bunge ya kuvunja mkataba wa kufua umeme kati yake na kampuni ya Dowans Holdings SA.

Kutoka Richmond hadi Symbion Power
KAMPUNI ya Marekani ya Symbion Power, imezuia chombo chochote kuchokonoa, kuchunguza na kutoa habari kuhusu mkataba wake wa ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans Costa Rica.
Malipo Dowans ni marafiki wanaolipa marafiki
RAIS wangu tukubali kuwa kikombe cha Babu Mchungaji Ambilikile Mwasapile wa Sumunge, Loliondo kinatibu maradhi mengi kuliko aliyoyataja na anayoyafahamu.

Symbion isijiingize kwenye tope la Dowans
PAMOJA na kwamba hatuna mashaka na uwezo wa kampuni ya Symbion Power LLC inayodai kuwa imenunua mitambo ya kampuni ya Dowans kuweza kuzalisha umeme, lakini ukweli ni kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kampuni hiyo kutumbikia katika mgogoro mkubwa wa kisiasa na hata kisheria.

Makamba kapata wapi uwezo kunyamazisha wananchi?
MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, January Makamba, amenaswa kwenye ndoana za kampuni ya kufua umeme ya Symbion Power LLC.
Ni zaidi ya miezi sita sasa tangu Makamba ajipe sura ya “ofisa uhusiano” wa makampuni ya kufua umeme ya Richmond Development Company (LLC), Dowans Holdings SA, Dowans Tanzania Limited (DHL) na sasa Symbion Power.
Aidha, hii ni mara ya pili tangu Makamba achaguliwe kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kupiga marufuku wanasiasa kuingilia mradi wa kuzalisha umeme wa Richmond na dada yake Do

Furaha ya Rostam kuzimwa?
SHIRIKA la umeme la taifa (TANESCO) limetupa kete muhimu likilenga kusimamisha ulipaji tozo ya Sh. 94 bilioni kwa mbunge wa Igunga na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC-CCM), Rostam Aziz kupitia kampuni ya Dowans Holdings SA, MwanaHALISI limeelezwa.

Rostam aingiza mkenge TANESCO
MPANGO wa wamiliki wa kampuni ya Dowans kuizunguka serikali na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ili kujinufaisha kiuchumi umegundulika.

Mikataba ya Mwinyi, Kikwete kufilisi nchi
VIONGOZI walioingiza serikali katika mikataba mikubwa mitatu ya utata, wameliandalia taifa mzigo mkubwa wa madeni yasiyolipika hata katika miaka 50 ijayo, MwanaHALISI limeelezwa.

Dowans rushwa tupu
- Siri za mawakili wao zavuja
- Wahofia TANESCO kushinda
Taarifa zinasema hoja ya kuwapo rushwa katika mkataba kati ya Dowans na TANESCO zilitosha kuishawishi Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), kutupilia mbali madai ya kampuni hiyo.

Misingi ya kutaifisha Dowans hii
KUNA hoja mbili kuu za kisheria zinazoweza kutumika kutaifisha mitambo ya kampuni ya kufua umeme ya Dowans. Kwanza, kutaifisha kwa kulipa fidia. Pili, kutaifisha bila kulipa chochote.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imeweka “Malengo muhimu na misingi ya mwelekeo wa shughuli za serikali kuwa ni pamoja na ustawi wa wananchi.”
Katiba pia imewapa wananchi haki mbalimbali na wajibu. Kwa mfano, ibara ya 24(1) ya katiba inatoa haki ya kumiliki mali na hifadhi ya mali hiyo na “...

Visa, vituko na filamu ya ziara ya Al-Adawi
WATUNZI wa filamu ni watu makini sana. Hupanga visa vikasisimua; huteua wahusika kulingana na nafasi zao; na huchagua maeneo ya kuigizia ili kusawiri kinachoelezewa na filamu yenyewe.

Rostam aiweka serikali mfukoni
ANAYEJIITA mmiliki wa makampuni ya Dowans ametua nchini kibabe kwa shabaha ya kutisha serikali, MwanaHALISI limeelezwa.
Mmiliki Dowans aja na mazingaombwe
BRIGEDIA Jenerali mstaafu, Suleiman Mohammed Yahya Al Adawi, anayetajwa kuwa mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya Dowans Holdings SA ameongeza utata nchini.

January Makamba ni wakala wa Dowans?
BABA wa Taifa Mwalimu Nyerere, katika moja ya hotuba zake alisema, ikulu ni mahali patakatifu. Alitumia neno ‘takatifu’ si kwa bahati mbaya. Kamusi inazungumzia neno hilo kama kitu kisichokuwa na dhambi, kilichotakasika.

Kikwete kataa kuwalipa kina Rostam
WAHUSIKA wawili wakuu katika sakata la mkataba tata wa kufua umeme wa dharula kati ya shirika la umeme la taifa (TANESCO) na kampuni ya Dowans – Suleiman Al Adawi na Rostam Aziz ambao mara kadhaa wamekana kufahamu lolote juu ya kampuni hiyo, sasa wamejitokeza hadharani na kujitambulisha kuwa ndio wamiliki halisi wa Dowans.

Tutaifishe mitambo ya Dowans
SPIKA wa Bunge la Jamhuri, Anna Makinda hakuwa na sababu zozote za msingi kukataa kusudio la kujadili bungeni hukumu ya mahakama ya kimatifa kati ya usuluhishi wa migogoro ya kibiashara (ICC) kati ya serikali na makampuni ya Dowans Holdings S.A na Dowans Tanzania Limited.

Mahakama: Rostam anakamatika
SIRI kuhusu ushiriki wa Rostam Aziz, mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mbunge wa Igunga, katika ufanikishaji mkataba tata wa Dowans, zinazidi kuanikwa.

Rai ni wazushi, wachonganishi
MCHAPISHAJI wa gazeti la MwanaHALISI, Saed Kubenea, amekana tuhuma kwamba gazeti lake linashiriki “njama za kupindua serikali ya Rais Jakaya Kikwete.”

Mafisadi wanatusingizia uhaini
WAZIRI mkuu Mizengo Pinda aliposema mafisadi ni hatari, wachambuzi wa masuala ya kisiasa walimrukia na kudai ni kauli ya kusalimu amri.

Rostam azidi kuanikwa
SIRI imefichuka. Kampuni ya Dowans Holdings SA inayodaiwa kusajiliwa nchini Costa Rica, haikuwa na “biashara nyingine yeyote duniani” wakati ikimpa Rostam Aziz mamlaka ya kisheria (Power of Attorney) ya kuiwakilisha nchini Tanzania.

Kama na yeye hajui, nani atajua?
IMERIPOTIWA kwamba Rais Jayaka Kikwete amesema naye hajui ni nani wamiliki wa kampuni ya Dowans. Kikwete hakusema tu kuwa haijui, lakini alisema jambo jingine linalotatiza wengi.

Kikwete na Dowans: Bado ni mchezo wa kuigiza
RAIS Jakaya Kikwete amekubali hadharani kuwa kampuni ya kufua umeme ya Richmond ilikuwa “kampuni hewa” na kwamba kampuni ya Dowans ilirithi mkataba wa kufua umeme wa kampuni feki.

Kikwete anasubiri sauti ya Mungu
WAPO baadhi ya maofisa wanaojaza fomu za safari na tiketi kama sheria inavyotaka katika kuonyesha wamesafiri ili walipwe nauli na posho za safari. Kumbe hawajasafiri.

Kikwete, Rostam, Lowassa, Karamagi wadaiwa Dowans
HATIMAYE kampuni ya Dowans Holding SA imesajili mahakama kuu nchini tuzo yake ya Sh. 94 bilioni iliyodondoshewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC).

Anayedai mabilioni ya Dowans ni Rostam
MJUMBE wa Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rostam Aziz, ndiye alishitaki serikali na ndiye anaidai Sh. 94 bilioni katika kesi ya Dowans, MwanaHALISI limebaini.

Kikwete njia panda
- Ukimya wake sasa wamponza
- Wabunge CCM wamkoromea
SUALA la kampuni ya kufua umeme ya Dowans limemweka Rais Jakaya Kikwete njiapanda, MwanaHALISI limeelezwa.

Wabunge na ‘madarasa mawili’
JANA wabunge walitarajiwa kuanza mafunzo ya siku 10 mfululizo. Wapya watakuwa wakijifunza: a e i o u za bunge. Wale wa zamani watakuwa wakiambiwa kuachana na mazoea.
Dowans wasilipwe
WANASIASA wanataja Dowans. Wanaharakati wanataja Dowans. Vyombo vya habari tunataja Dowans.

Wakiwalipa Dowans, tuwalipishe
NINAZO habari mbili; moja mbaya nyingine nzuri. Kwanza, ni mkataba ambao Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO) ilifunga na kampuni ya Richmond na kujiweka chini ya usuluhishi wa Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi (ICC) bila ya kuwa na nafasi ya kukataa rufaa.