Richmond
Mlolongo wa Habari za kashfa ya Richmond

Lowassa kuibukia bungeni
- 'Majemedari' wake wajipanga
- Kikwete huenda akahusishwa
EDWARD Lowassa, aliyekuwa waziri mkuu, anatarajiwa kuibukia katika mkutano ujao wa Bunge na kupasua kile kinachoitwa "ukweli kuhusu utata wa mkataba wa Richmond," imefahamika.

Lowassa, Msabaha hapatoshi
- Ni katika sakata la Richmond
- Kila mmoja apanga kujinasua
HATMA ya Edward Lowassa kujinasua kwenye kashfa ya mkataba tata wa kampuni ya Richmond, ipo mikononi mwa Dk. Ibrahim Msabaha, MwanaHALISI limeelezwa.

Lowassa anajua uzalendo au ni ‘machozi ya mamba?’
EDWARD Lowassa, yule aliyejiuzulu nafasi ya waziri mkuu kutokana na kashifa ya kuingiza nchi kwenye mkataba wa kinyonyaji wa makampuni ya Richmond/Dowans, sasa anasaka utakaso.

Mjadala wa Richmond urejeshwe tena bungeni
RIPOTI ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba tata kati ya serikali na kampuni ya kufua umeme wa dharula ya Richmond Development Company (RDC), hatimaye “imekamilika.”
Kikwete mtuhumiwa, tufanye nini?
UKURASA mpya kuhusu sakata la Richmond, umefunguliwa baada ya mambo mawili kutokea katika vikao vya Chama Cha Mapinduzi (CCM), vilivyomalizika mjini Dodoma Alhamisi iliyopita.
Zimwi la Richmond bado lamuandama Lowassa
VIONGOZI waliokuwa serikalini wakati wa mkataba wa kuzalisha umeme wa dharula wa Richmond bado wanaendelea kung’ang’aniwa kwenye kashifa ya kushiriki kwenye ufisadi wa mkataba huo, MwanaHALISI limeelezwa.

Lowassa amchokoza Kikwete
EDWARD Lowassa, waziri mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, “amemtia kidole jichoni” Rais Jakaya Kikwete.

Symbion: Mwanzo au mwisho wa kashfa?
SERIKALI ya Rais Jakaya Kikwete iliridhia mapendekezo ya Bunge ya kuvunja mkataba wa kufua umeme kati yake na kampuni ya Dowans Holdings SA.

Kutoka Richmond hadi Symbion Power
KAMPUNI ya Marekani ya Symbion Power, imezuia chombo chochote kuchokonoa, kuchunguza na kutoa habari kuhusu mkataba wake wa ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans Costa Rica.

Rais Kikwete hajamchoka Mrindoko?
WIKI iliyopita, Rais Jakaya Kikwete alifanya uteuzi wa naibu makatibu wakuu wapya 10 katika wizara mbalimbali ndani ya serikali yake. Miongoni mwa walioteuliwa, ni Bashir Mrindoko aliyefanywa naibu katibu mkuu wizara ya maji.

Lowassa hasafishiki
JUHUDI za waziri mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, kujisafisha mbele ya jamii, zimegonga mwamba baada ya kubainika kuwa ni serikali iliyoingiza kampuni ya Richmond katika mkataba wa kufua umeme.

Richmond bado yamwandama Lowassa
KATIKA kile kinachoitwa “maandalizi ya kuelekea ikulu,” waziri mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya mkataba tata wa Richmond, Edward Lowassa ametungiwa kitabu cha kumsafisha.

Misingi ya kutaifisha Dowans hii
KUNA hoja mbili kuu za kisheria zinazoweza kutumika kutaifisha mitambo ya kampuni ya kufua umeme ya Dowans. Kwanza, kutaifisha kwa kulipa fidia. Pili, kutaifisha bila kulipa chochote.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imeweka “Malengo muhimu na misingi ya mwelekeo wa shughuli za serikali kuwa ni pamoja na ustawi wa wananchi.”
Katiba pia imewapa wananchi haki mbalimbali na wajibu. Kwa mfano, ibara ya 24(1) ya katiba inatoa haki ya kumiliki mali na hifadhi ya mali hiyo na “...

Rostam aiweka serikali mfukoni
ANAYEJIITA mmiliki wa makampuni ya Dowans ametua nchini kibabe kwa shabaha ya kutisha serikali, MwanaHALISI limeelezwa.
Mmiliki Dowans aja na mazingaombwe
BRIGEDIA Jenerali mstaafu, Suleiman Mohammed Yahya Al Adawi, anayetajwa kuwa mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya Dowans Holdings SA ameongeza utata nchini.

Tutaifishe mitambo ya Dowans
SPIKA wa Bunge la Jamhuri, Anna Makinda hakuwa na sababu zozote za msingi kukataa kusudio la kujadili bungeni hukumu ya mahakama ya kimatifa kati ya usuluhishi wa migogoro ya kibiashara (ICC) kati ya serikali na makampuni ya Dowans Holdings S.A na Dowans Tanzania Limited.

Kikwete na Dowans: Bado ni mchezo wa kuigiza
RAIS Jakaya Kikwete amekubali hadharani kuwa kampuni ya kufua umeme ya Richmond ilikuwa “kampuni hewa” na kwamba kampuni ya Dowans ilirithi mkataba wa kufua umeme wa kampuni feki.

Bunge limjadili Rais Kikwete
ALHAMISI ya 20 Januari 2011, Rais Jakaya Kikwete alifanya kazi mbili nzito mchana na usiku; moja yenye maslahi kwa taifa na nyingine yenye tija kwa mafisadi.
Wamiliki wa Dowans wanafahamika
KWA MUDA mrefu sasa, jamii na vyombo vya habari vimekuwa vinashinikiza serikali imtaje mmiliki au wamilki wa kampuni ya Dowans ambayo ilishinda kesi hivi karibuni dhidi ya serikali na kuamriwa ilipwe Sh. Bilioni 185.
Ya Dowans ni kashfa nyingine serikalini
HAKUNA ubishi kwamba uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara (ICC), unaotaka serikali kulipa Dowans fidia ya Sh.185 bilioni, ni hujuma kwa taifa na kashfa nyingine ndani ya kashfa.

Nani anayekabidhiwa fedha ya Dowans?
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri, Mizengo Pinda amejitwisha zigo lisilobebeka. Litamuangusha. Ameahidi kulipa mabilioni ya shilingi kwa kampuni ya kufua umeme wa dharula, Dowans Holding Tanzania Limited.

Dowans kuifilisi Tanesco
SHIRIKA la Umeme nchini (Tanesco) liko hoi kiuchumi na halikopesheki, MwanaHALISI imeelezwa.

FIDIA DOWANS: Wizi uleule, wezi walewale katika suti mpya
WATUHUMIWA wakuu wa ufisadi nchini wanashangilia. Waliojiita wapambanaji, wanazomewa. Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO), linajikuta lipo katikati na sasa linalazimika kutii agizo la mahakama.

KKKT na mzimu wa Richmond
MKUTANO mkuu wa Kanisa la Kiinjili na Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, umemalizika mjini Bagamoyo kwa staili ya aina yake. Ni fedha chafu kushindwa kufanya kazi kwa waliomtanguliza Mungu mbele.

Sitta amtikisa Kikwete
HATUA ya kumuengua aliyekuwa spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta kwenye kinyang’anyiro cha uspika, ililenga kusafishia njia aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, MwanaHALISI limeelezwa.

Richmond: Kufunga mjadala bungeni ni kukejeli umma
BUNGE la Jamhuri limetishwa. Spika Samwel Sitta “ameng’olewa meno” na kurejeshwa katika “dini” yake ya asili.

'Mitume kumi na mbili' imevuna au imepoteza?
- SAKATA LA RICHMOND
HOJA za msingi hazijajadiliwa. Watuhumiwa wa ufisadi wameendelea kupeta. Vidonda vya migawanyiko vilivyokuwa vipate tiba, vimeshindikana kupona.

Mjadala wa Richmond bado haujafungwa
MJADALA juu ya mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura kati ya serikali na kampuni ya kitapeli ya Richmond Development Company (LLC), ungali mbichi.

Richmond yaibabua serikali
RIPOTI ya serikali kuhusu Richmond ni "chafu" na huenda isiwasilishwe mbele ya bunge zima, imefahamika.

Kauli ya Rostam Aziz haivurugi serikali?
ZIMWI la mkataba kati ya serikali na kampuni ya Richmond Development Company (LLC) bado linaitesa serikali; lakini zaidi linamzonga Rostam Aziz.