Yanga
Mlolongo wa Habari zinazohusu Klabu ya Yanga

Fursa pekee kwa Yanga kuandika ukurasa mpya
HUU ni wakati wa wanachama wa klabu ya Yanga, Dar es Salaam kuandika ukurasa mpya baada ya mkutano uliomalizika kwa ‘kuufurusha’ uongozi wa Mwenyekiti, Imani Madega.
Haya ni madudu ya kamati ya uchaguzi Yanga
JUNI 6, mwaka huu mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Imani Madega aliitisha mkutano mkuu wa kujadili marekebisho ya katiba, lakini mwishoni akaporwa madaraka na kamati ya uchaguzi.

Matola: Kisago cha Yanga mazoezi kwa Waarabu
KISAGO cha mabao 4-3 ilichotoa Simba kwa watani wao wa jadi katika soka, Yanga ni kipimo tosha juu ya uwezo wa timu hiyo ya Msimbazi kabla ya kuumana na Haras El Hadood ya Misri katika Kombe la CAF.

Nani anasema safari ya Yanga itaishia kwa FC Lupopo DRC?
NI ukweli usiofichika kwamba, nyoyo za mashabiki wa soka nchini, hasa wale wa Yanga zimetumbukia nyongo baada ya kipigo cha mabao 3-2 mwishoni mwa wiki mbele ya FC Saint Eloi Lupopo ya Lumbumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Asante Phiri, Papic
ASANTE kocha wa Simba Patric Phiri. Asante kocha wa Yanga Kostadin Papic kwa kutufundishia timu zetu zikaweza kucheza mpira nzuri wa kuvutia.

Naitamani ndoa ya Yanga, Papic
NIANZE kwa kuwatakia Kheri ya Mwaka Mpya kwa wote waliobahatika kupita katika chujio la Mwenyezi Mungu na kuuona mwaka 2010.

Yanga ni Manji, Madega na wenzake wana nini?
NIMEKUWA nikijiuliza mara kwa mara majukumu ya viongozi wa Yanga tangu kuingia kwa mfadhili mkuu wa klabu hiyo, Yussuf Mehboob Manji.

Yanga, Mungu awape nini tena?
NIANZE kwa kuupongeza uongozi wa Yanga, chini ya Mwenyekiti Imani Omar Madega kwa kuamua kuachana na ubabaishaji, na hatimaye kuonekana kushika njia sahihi ya uendeshaji wa kisasa wa klabu.

Simba, Yanga na ushiriki wao kuiua Taifa Stars
MEI 3 mwaka huu, Shirikisho la Soka Misri (EFF), lilipitisha uamuzi wa kuzizuia klabu za nchi hiyo kusajili makipa kutoka nje ya nchi hiyo, kuanzia msimu ujao wa ligi.

Yanga na mwelekeo wa kufufuka!
KUNA wakati ilikuwa ni jambo la kawaida kuona viongozi wa klabu kubwa za Simba na Yanga wakichomekea katika usajili majina ya watoto au hata ndugu zao wa karibu.

Kuhusu Kaseja, Kondic asidanganye Yanga
UMESHIKA gazeti hili ulipendalo la MwanaHALISI. Unasoma makala hii. Aya ya tano tu za kwanza, fumba macho. Tafakari na vuta hisia juu ya kipa bora nchini Tanzania.

Madega alipania "kuiuza" Yanga
SAFARI ya Yanga katika michuano migumu, yenye mvuto na utajiri mkubwa wa fedha katika ngazi za klabu barani Afrika, Ligi ya Mabingwa imefikia mwisho.

Yanga: Mbinu au woga kwa Ahly?
KITENDAWILI cha Yanga cha ama kuendelea na safari ya kuusaka ubingwa wa Afrika au kurudi mchangani kusubiri ratiba ya mwaka 2010, kinatarajiwa kuteguliwa Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Kwa maandalizi haya, siku zote tutaishia kuwa watalii
KLABU ya Yanga ya Dar es Salaam, mwakilishi pekee nchini aliyebaki katika michuano ya vilabu barani Afrika, ilipata kipigo cha mabao 3-0 mbele ya Al Ahly ya Misri zilipokutana 15 Machi mjini Cairo.

Madega na vita ya Yanga kwa Ahly
PRESHA inapanda, presha inashuka. Kwa hakika ndiyo hali inayoweza kufikirika kwa sasa miongoni mwa mashabiki wa klabu za Yanga na Al Ahly ya Misri.

Yanga na siku 38 za kuiua Al Ahly
USHINDI wa Yanga wa mabao 8-1 dhidi ya Etoile d'Or Mirontsy ya Comoro ni ishara tosha kwamba, wakali hao wa makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, pale Kariakoo, Dar es Salaam wameshamaliza ngwe ya kwanza ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika inayoongoza kwa utajiri mkubwa wa fedha, utitiri wa vipaji na mvuto.

TFF wanajua sababu za Yanga kususia
KLABU ya Yanga iliyoingia kwenye michuano ya klabu bingwa ya Afrika Mashariki na Kati kama timu ya pili iliyotokana na Tanzania Bara kuwa wenyeji wa michuano hiyo, inaambiwa imehujumu michuano.

Manji anadhamira na Yanga?
KWA mwanayanga yeyote, ni lazima atakuwa anatembea kifua mbele kutambia usajili wa kufuru uliofanywa na bilionea kijana mwenye umri wa miaka 30 tu! Yusuf Manji.

Yanga sasa ikuwe!
NIANZE kwa kuipongeza Yanga kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara msimu huu.