FUNUNU na malalamiko juu ya upangaji matokeo katika mechi za Ligi Kuu ya Bara huwa yanapuuzwa kwa madai ya kukosekana ushahidi. Klabu ndogo za soka zimekuwa zikilalamika kwamba Yanga na Simba zinabebwa, lakini hazisikilizwi.
Leo, hiki kilichotokea katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, Zanzibar kinathibitisha klabu hizo kongwe katika soka nchini zinabebwa. Wakati kila shabiki ameona na amesikia, waandaaji michuano wameamua kufumba macho.
Mashahidi ni makocha Salum Bausi wa Miembeni na Stewart Hall wa Azam FC, na kiongozi wa klabu ya Miembeni.




