Recent comments


  • Kulingana na mazingira ya bunge letu, Je Samwel Sitta amewezea uspika?   2 weeks 6 days ago

    Ameweza kusimamia ukweli kwa uwazi mkubwa....

    Jacob
  • Tunataka mdahalo wa wagombea urais   3 weeks 4 days ago

    Mimi binafsi ninaunga sana mkono mdahalo kati ya wagombea urais hao watatu, na hata ikiwezekana wawe wengi zaidi ya hao. Ila cha msingi ni vyema mgombea urais kupitia CCM, ambacho ndicho kilichopo madarakani, akawepo. Cha kushangaza ni kwamba wasemaji wa CCM, Makamba na Hiza wamesema Kikwete hawezi kushiriki kwa sababu zifuatazo:
    1. Akishiriki atakuwa anawapigia debe (anawatangaza)wagombea wapya (kutoka upinzani)
    2. Wananchi wanajua mambo mengi mema na ya maendeleo aliyotekeleza wakati wa utawala wake wa miaka mitano
    3. Kufuatana na Makamba, Kikwete anavijua vyema vita na ameshapigana kwa mafanikio. Wagombea kutoka upinzani, 'hawana kitu mkononi' - hawana cha kuwaambia wananchi.

    Sasa kama Kikwete ameleta maendeleo makubwa nchini, anakubalika, na ni mzoefu wa Ikulu, anachoogopa mdahalo ni nini?

    Atapoteza fursa ya maana sana akifanya hivyo, na wanaomshauri kuuukimbia mdahalo, wasijejutia kitendo hicho baada ya uchaguzi Oktoba. Historia inatueleza vyema kuwa wengi wa waliokacha midahalo muhimu kama hii, waliwapa walioshiriki fursa ya kumjadili katika kutokuwepo kwake, na hawezi tena kurudi na kujadili yale yatakayokuwa yamesemwa juu yake.

    Nimshauri Kikwete 'akili yake kuichanganya na ya Makamba na HIza, kisha kuamua kwa kutumia zaidi akili yake'

    Mdahalo uendelee na tena uvume kwa kishindo katika vyombo mbalimbali vya habari ili majadiliano muhimu kama hayo yawafikie wananchi ko kote walipo.

    Stella Damaris
  • Kulingana na mazingira ya bunge letu, Je Samwel Sitta amewezea uspika?   6 weeks 6 days ago

    Alifanya vizuri sana na aliweza kusimamia ukweli na ubora wa bunge letu kwenye habari muhimu za kitaifa

    Papa
  • Kikwete amtema rasmi Lowassa   9 weeks 6 days ago

    Kama haya yatajiri, CCM inaipeleka wapi nchi? Viongozi hawachaguliwi tena kulingana na ubora wa uongozi wao? Hebu tuamini kuwa aina hii ya urithi wa madaraka hautatokea; vinginevyo tujiandae na 'usultani wa madaraka' Akitoka Karume atampisha Shein, naye Shein kwa kulipa fadhila atampisha Ridhiwani ambaye kwa wakati huo watasema amekomaa kisiasa.

    Mtandao na makundi ndani ya CCM vitamalizwa kwa vikao vyenye dhati ya kujadili na kukemea maovu yatendwayo ndani ya CCM, na si kuanzisha usultani wa uongozi ndani ya chama.

    Stella Damaris
  • Lowassa amhujumu Mwandosya   11 weeks 17 hours ago

    MWENYEZIMUNGU AKUPENI AFYA NJEMA NA UJASIRI NYIE WAANDISHI WAKAKAMAVU MSIOOGOPA NGUVU NA MAPESA YA MAFISADI

    SALMAN
  • Lowassa atajwa tena   13 weeks 14 hours ago

    Rudi Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere. Mbona uliondoka mapema? Mbona umetuachia viongozi wanaotengeneza ufalme na usultani wa U-rais? Wao na watoto wao wamegawana madaraka ya kile chama ulichokipigania sana. Wako pia kule Ikulu. Huko ndiko wanakopangia mikakati ya kuhujumiana. Ni kinyume! Wewe ulitumia Ikulu kujenga misingi ya maendeleo ya Taifa. Baba wa Taifa, hata wewe ulikuwa na watoto lakini si wewe wala watoto wako mliopanga mkakati wa kupeana vijiti vya uongozi. Hata kama kijana wako aliingia Bungeni, aliingia kupitia mlango wa jirani, si kupitia mlango wa nyumba yako Baba wa Taifa. Ilikuwa marufuku! Nisikie na uniamini, taifa lako halina tena viongozi, bali kuna wafalme na masultani wa U-rais na Chama. Rudi Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere!

    Stella Damaris
  • Ridhiwani, Januari walikwina?   14 weeks 14 hours ago

    VIONGOZI WETU WANA ULEVI MBAYA SANA JUU YA MADARAKA NAFIKIRI MPAKA WATOTO WAO HUKO MASHULENI WANAWAHIMIZA WAGOMBEE URANJA MAANA ILIKUWA AIBU UCHAGUZI WA WATOTO KULE MOROGORO,MTOTO WA KIKWETTE KACHAGULIWA BILA KUWEPO UKUMBINI,WAPI TUNIPELEKA NCHI HII

    SALMAN
  • Tayari uchaguzi mkuu umevurugwa   14 weeks 15 hours ago

    Ninatamani Waziri Jumanne Maghembe awe amesoma makala hii. Utetezi aliotoa unamfaa nani? Na kwa majibu yake mepesi kwa maswali magumu yanayohitaji majibu makini, labda tumwambie Waziri tu kuwa hawezi kuwadanganya watu wote wakati wote.

    Stella Damaris
  • Ridhiwani, Januari walikwina?   14 weeks 16 hours ago

    Ridhiwan January walikwina?

    Makala hii ni ushauri wa bure na wa busara kwa walengwa. Mwenye masikio na asikie.

    Hawatasikia japo wana masikio kwa sababu ya tamaa walizokwishajiwekea mioyoni mwao. Ni Opportunists hawa!!

    Stella Damaris
  • Simu ya Rais haina tija   15 weeks 2 hours ago

    Inasikitisha rais wa nchi kukesha usiku akidonoa donoa simu yake eti anajaribu kuwa karibu na wananchi. Inaelekea akili ya rais wetu ni kama ya mbongo wa kawaida tu asiyejua kwamba matatizo tunayoyapata yanatokana na viongozi wetu kuzembea kazi wakitumia muda mwingi kujipanga kwa ajili ya maslahi yao. Hamna mtu anayetaka kuwa responsible bado tunasubiri maendeleo yaletwe na Nyerere. Lakini tusimlaumu sana maana ni sisi ndio tuliomchagua kwa kishindo na bado tutamchagua tena. Ataendelea kubembea mpaka hapo watanzania tutapong'amua kwamba kura ni silaha inayopaswa kuheshimiwa na kutumiwa vizuri.

    mbangaizaji
  • Safari za Kikwete zakausha hazina   15 weeks 2 days ago

    we have to take a chance as public to advice the government,even by doing media debate may be our non directional government can change,or revolution if possible

    kalemera
  • Kikwete achemka   17 weeks 18 hours ago

    Maisha ni magumu sio tu kwa wafanyakazi kwenye taasisi za serikali na makampuni ya umma au binafsi.
    Gharama za maisha zimepanda na huduma hazitosherezi mahitaji au matakwa ya wananchi walio wengi.
    Tukubali au tusikubali Tanzania ina matatizo ambayo mengi tunao uwezo wa kuyatatua sisi wenyewe bila misaada kutoka nje.
    Mishahara au kipato cha kukidhi mahitaji tunaweza bila kukumbatia wafadhili na makampuni ya kibepari.
    Tupanue wigo wa mapato ya serikali na tudhibiti mapato ya serikali. Tupunguze matumizi ya kiwendawazimu ya kujitanua kama mataifa makubwa.
    Ifike wakati ziara za viongozi wetu kwenda nje sio kuomba misaada tu bali hata kuchangia maendeleo ya mwanadamu kwa ujumla.
    Nina huhakika serikali ikijipanga vizuri ina uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyakazi na marupurupu bila kuteteleka.

    sblandes
  • Kikwete achemka   17 weeks 23 hours ago

    Kwa hili la Rais kudanganywa kwa mara nyingine tena, hapana sasa ifike mahali iwe hapana!. Tujiulize huyu Rais ni mtu wa aina gani kiasi kwamba yeye anadanganywa mara kwa mara? Hajitambui? Haoni kama anajidhalilisha mwenyewe? Huenda ana matatizo Rais wetu, na sisi wananchi wake tunaendelea kumlaumu tu bila kujua. Hapana, kwa hapa tulipofika, hapana!

    Stella Damaris
  • Kikwete achemka   17 weeks 1 day ago

    Kweli rais huyu anaitaji kuombewa jamani. Tufunge na kusali habadilike. Inawezekana

    Papa
  • Pigo MwanaHALISI   17 weeks 2 days ago

    Pole kwa Watanzania wote kumpoteza mtu muhimu kama huyu, pole pia kwa uongozi wa Mwanahalisi kuondokewa na mwanataaluma mwenzao.
    Hakika nafasi yake kuzibika ni vigumu hasa kipindi hiki ambapo wanataaluma wanaochipukia wameweka pembeni maadili ya taaluma.
    Mungu ailaze mahali pema roho ya ngugu yetu Konga.

    archard
  • Rostam aibiwa   17 weeks 3 days ago

    Hongereni kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kutoa habari za ukweli zisizo na upendeleo kwa mtu yeyote. Mmekuwa mwanga kwa watanzania wengi wapenda maendeleo. Tunaomba mjitahidi kuwahisha gazeti lenu kwenye mtandao, kwanikwa sasa linachelewa sana kuwekwa kwenye mtandao.

    Ahsanteni na endeleeni na kasi hiyo hiyo ya kutoa habari

    Noel Peter Sawe
  • Rostam aibiwa   17 weeks 4 days ago

    Wanaochagua Mafisadi watajiju hiki sio kipindi cha kusaidiwa na Mafisadi. Unatakiwa uchague watu makini wa kukutoa kwenye lindi la umasikini.Hakuna Fisadi anataka mufanane hata siku moja.Wao wanataka uwapigie magoti maisha yako yote.

    LENGAI OLE LETIPIPI
  • Serikali bado iko ‘chekechea’   17 weeks 5 days ago

    Tatizo letu nini?ni elimu isiyotoshoreza matakwa ya jamii yetu au ni vichwa vibovu.Kama ni elimu yetu inawalakini tufanye nini?
    Kama ni vichwa vibovu uhuru tuliomba wanini?Au ni laana kutoka kwa Mweyezi Mungu?
    Au ni kutoelewa mbinu za kibepari maanake miaka mingi tulikuwa na serikali ya kijamaa?
    Tuwache kuendesha nchi kishabiki turudi kwenye drawing board,uozo na ubutu wa mikataba ni nyingi kiasiinatia kichefuchefu.
    Kashafa ,uzandiki,wizi,uvujaji wa mali ya umma ni kama milipuko ya volcano.
    Bunge limekuwa kubwa lakini halina uhodari wa kutunga sheria.
    Kila kukicha majimbo ya uchaguzi na wilaya zinaongezwa sio kumletea mwananchi maendeleo bali kumuongezea gharama za uendeshaji.Mwenye macho haambiwi tazama.Hivi huyo Baba wa Taifa mlikuwa mnamelewa au mlikuwa wavivu wa kujifunza a,e,i,o,u.

    sblandes
  • Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ulikuwa Huru na Haki?   17 weeks 5 days ago

    Na mimi leo nakubaliana na stella kwamba gazeti hili sisi wa mbali tunachelewa kulipata kwenye hard copy kwahiyo tunaomba mtuwekee kwenye soft copy basi, kwa maana leo jumatatu ndio nasoma gazeti la jumatato kweli tunapitwa na habari nyingi

    Mhariri tunakuomba utufikirie hilo la kuwekea gazeti kwenye internent soft copy.

    Joseph Mushi
  • Serikali bado iko ‘chekechea’   17 weeks 6 days ago

    DAAAH NCHI HII NIMESHAKATA TAMAA NA NCHI HII,MAANA WATU KADRI WANAVYOELIMISHWA KUHUSU UBAYA WA CCM NDIO KWANZA WATAIPA KURA YA KISHINDO MWEZI OCTOBA,MIE NINGESHAURI VIONGOZI WA DINI WANGEENDESHA MAOMBI YA MWEZI MZIMA MUNGU ATUANGAMIZE WATANZANIA WANAFIKI WOOTE,AWABAKIZE WANAFUNZI WA VYUO VIKUU,NA WATOTO WETU WAANZE KUIJENGA TANZANIA YENYE NEEMA,LAKINI TUKITEGEMEA BALLOT BOX CCM ATATAWALA MIAKA 7000

    SALMAN
  • Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ulikuwa Huru na Haki?   18 weeks 19 hours ago

    Mwanahalis Big Up, Your news paper Now looks similar to Newyork Times in the website. You are great thinkers and informers. Keep it up.

    Papa
  • Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ulikuwa Huru na Haki?   18 weeks 4 days ago

    Acha nimwunge mkono Joseph Mushi hapo juu kwamba ninalipenda sana gazeti hili.Tatizo ni moja tu - haliwekwi kwenye mtandao kwa wakati mwafaka sisi tulio mbali na nyumbani tukalisoma kwa wakati unaofaa. Hatuwezi kuifikia 'hard copy', tunategemea mtandao kusoma habari za nyumbani. Ndugu Mhariri, tukumbuke na sisi tulio mbali na upeo wa macho ya Tanzania kwa kuliweka gazeti lako mahiri hapa mtandaoni.

    Stella Damaris
  • Rais Kikwete aumbuka   18 weeks 6 days ago

    nadhani kila aliyeweka maoni yake amekuwa na jambo moja kubwa nalo ni kuweka matoleo ya gazeti la wiki mapema. naelewa pia kwa upande wa kibiashara mnakuwa na wasi wasi lakini ukweil unabaki kuwa njia za kuuza matangazo zipo na kama mnavyoelewa kuwa gazeti lenu lina wasomaji makini kwahiyo mnaweza kabisa kuwashawishi makampuni mbali mbali yakatangaza kwenye tovuti yenu na nyie mkapata pesa ziada lakini pia kumbuka kuwa wenye nia njema na wenye kuwa na umakini hawapo Tanzania peke yake lakini ni watanzania tena naweza kusema Watanganyika wa ndani kabisa wenye uchungu na nchi yao tafadhalini msiwanyime fursa ya kuona matukio kwa wakati na kusoma habari kwa wakati hivyo jitahidini kuweka matoleo kwa wakati na inawezekana kikubwa ni nia tu
    Ahsante

    King Mbega
  • Rais Kikwete aumbuka   19 weeks 3 days ago

    Inawezekanaje Rais akasign such an important piece of legislation bila kusoma. Is it possible to absolve him of the blame given the amount of resources at his disposal?!! I think it is a case of complete negligence and incompetence. Raisi hayupo hapo kuletewa tu documents and sign. I dont think we elected a rubber stamp president who has no time to review the papers before him and sign without proper application of mind. If he has been doing so its high time we advise him to change.

    Matatizo ya kudanganywa na wasaidizi hayajaanza jana. There is enough evidence for that. What is troubling is after knowing that he still puts 100% in the same people and the through the same procedure!!

    It is embarrasing that the president becomes aware of the faulty provisions of a law in his party meeting and orders the re-examination of the same!. A serious question then needs to be asked on whether the proposed changes will not only benefit his party? Besides in his capacity in that meeting as the party chairman,did he even have the authority to order that? (Because that was a party meeting so he was not discharging his executive functions)

    The Critic
  • Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ulikuwa Huru na Haki?   19 weeks 4 days ago

    Napenda sana hili gazeti lenye uchambuzi wa kina lisilokuwa na ubabaishaji kabisa

    Joseph Mushi