Kikwete tumbo moto


Ezekiel Kamwaga's picture

Na Ezekiel Kamwaga - Imechapwa 29 December 2010

Printer-friendly versionSend to friend
Rais Jakaya Kikwete

HOFU imetanda serikalini ya kuanikwa kwa taarifa za mazungumzo ya siri kati ya Rais Jakaya Kikwete na viongozi wa serikali ya Marekani, MwanaHALISI limeelezwa.

Tayari mtandao wa WikiLeaks umevujisha mazungumzo ya siri kati aliyekuwa naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Jendayi Frazer na rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

MwanaHALISI limefahamishwa na vyanzo vyake ndani ya serikali kuwa Rais Kikwete aliwahi kukutana na Frazer mara kadhaa kati ya 2005 na 2010.

Katika mikutano hiyo, mtoa taarifa anasema, Rais Kikwete na Frazer walijadili mambo mengi yanayohusu Tanzania, Afrika na kimataifa.

Mkutano wa kwanza kati ya Kikwete na Frazer ulifanyika Jumatatu ya 17 Oktoba 2005, katika ofisi za wizara ya mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimatifa, jijini Dar es Salaam. Alikuwa hajawa rais.

“Bila shaka Kikwete amekuwa akimweleza mengi Frazer. Haya mambo yakiibuka leo, yanaweza kubomoa hadhi yake,” ameeleza kiongozi mmoja mwandamizi ndani ya CCM ambaye aliwahi kuwa waziri.

Anasema, “Unaju ndugu yangu, mazungumzo ya rais na Frazer yalifanyika katika mazingira ya kuaminiana sana kama ulivyo utaratibu wa kidiplomasia; kwamba kinachozungumzwa kinabaki siri ya wazungumzaji au ya mataifa yao. Sasa, unaweza kuona mwenyewe hatari iliyopo.”

Mtoa taarifa anasema wakati Kikwete anakutana na waziri huyo wa Marekani, ndio kwanza alikuwa amepitishwa na chama chake kuwa mgombea urais.

Anasema, “Nakuhakikishia kwamba kuna uwezekano mkubwa wa rais kuahidi mambo mengi ili kujijengea mazingira mazuri ya kukubalika kwa taifa kubwa kama Marekani.”

Akiongea kwa kujiamini, mtoa taarifa huyo amesema, “Rais lazima atakuwa amezungumzia msimamo wa serikali yake kimataifa na jinsi atakavyoshughulikia mambo ya ndani ya nchi.”

Anasema, “Rais anaweza kuwa aliahidi jinsi ya kushughulikia waasi wa Burundi, uhusiano wake na mataifa mengine ya Afrika, Komandi kuu ya kijeshi ya Marekani barani Afrika (Africom) na hata ubinafsishaji wa mashirika ya umma, mikataba ya madini, uwekezaji na mapambano dhidi ya rushwa.”

Kabla na baada ya Kikwete kuingia madarakani, waliojiita “wana-mtandao” walijiapiza kuwa mgombea wao angerejesha nyumba za serikali zilizouzwa kiholela na angerejesha mikononi mwa wananchi mashirika ya umma yaliyobinafsishwa kinyume cha taratibu.

Wachunguzi wa mambo wanasema inawezekana Kikwete alikwenda mbali kueleza jinsi atakavyokuwa na serikali imara, akitaja atakuwa na nani; na nani hawezi kumteua na kwa nini.

Kwa mujibu wa mmoja wa maofisa waliohudhuria mazungumzo hayo, Rais Kikwete alimweleza Frazer jinsi serikali ilivyopania kuhakikisha uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 unakuwa huru na wa haki.

Akijibu swali la naibu waziri huyo aliyetaka kujua nafasi ya CCM katika uchaguzi mkuu upande wa Zanzibar, Kikwete alisema, “Matokeo yatakuwa mazuri.”

Kuibuka kwa taarifa hizo kumekuja wiki moja baada ya Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), Edward Hoseah, kunukuliwa akimtuhumu Rais Kikwete kukwamisha utendaji wake wa kazi.

Taarifa za Hoseah kumtuhumu Kikwete zilipatikana katika mtandao wa WikiLeaks ukimnukuu mwanadiplomasia wa Marekani, Purnel Delly, ambaye alikutana faragha na Hoseah mwaka 2007.

Hoseah ambaye alikuwa mmoja wa wajumbe katika Kamati ya rais iliyopewa kazi ya kukusanya fedha zilizoibwa Benki Kuu ya Taifa (BoT), alinukuliwa na mtandao huo akisema, “Rais Kikwete hana dhamira ya kuwafikisha mahakamani walarushwa wakubwa nchini.”

Aliyekuwa waziri wa Utawala Bora, Sophia Simba aliuambia mkutano kati ya kamati ya wazee wa chama chake na wabunge, uliofanyika Novemba 2009 katika ukumbi wa zamani wa Bunge mjini Dodoma, kwamba ndani ya CCM hakuna aliyesafi.

Simba ambaye vyombo vya TAKUKURU na Idara ya Usalama wa Taifa vilikuwa chini yake, mbali na kueleza jinsi fedha zilizoibwa, alidai kuwa mmoja wa watuhumiwa wakuu wa wizi huo, Jeetu Patel alifadhili mbio za kusaka urais za John Malecela mwaka 2005.

Waziri huyo ambaye wakati huo ofisi zake zilikuwa ikulu, alikieleza kikao cha wabunge na wazee, “Hakuna mwenye ubavu wa kunyooshea kidole wengine.”

Alisema Jeetu alitoa kiasi cha Sh. 200 milioni na kumpa Malecela na kwamba kelele za Anne Kilango Malecela za kupiga vita ufisadi, zinatokana na kile alichoita, “Nongwa ya kuukosa u-first lady” – mke wa rais – iwapo Malecela angepata urais.

“Rais anayajua haya. Kuna uwezekano mkubwa kuwa tayari ameyamwaga kwa Marekani ili kujikwamua na shinikizo la wafadhili wanaomtaka kukamata watuhumiwa wa EPA,” anaeleza mbunge mmoja wa CCM kwa sharti la kutotajwa gazetini.

Amesema iwapo haya yatatoka, kwanza yatamgombanisha rais na wenzake, lakini pia, yatashusha hadhi yake kitaifa na kimataifa.

Anasema, “Hebu fikiria kama rais mwenyewe atanukuliwa akiwataja kwa ubaya watangulizi wake. Au akiwasema marais wa nchi jirani ambao anakaa nao kila siku. Je, hapo kutakuwa na kuaminiana kweli,” anahoji.

“Au kama alimwambia Frazer kuwa haridhiki na mawaziri wake fulani au hana imani nao… unadhani nini kitatokea kwenye baraza la mawaziri? Watu si wanaweza kumuacha peke yake?” kiliuliza chanzo hicho.

Mkutano mwingine muhimu kati ya Kikwete na Frazer ulifanyika Jumatano 16 Aprili 2008, katika Hoteli ya Intercontinental, jijini New York, Marekani.

Vyombo vya habari vya nchi za Magharibi, viliripoti kuwa ajenda kuu ya mkutano wao ilikuwa ni hali ya Zimbabwe na jinsi Umoja wa Afrika (AU) na Marekani zinavyoweza kusaidia kuhakikisha uchaguzi nchini humo unafanyika chini ya misingi ya amani na haki.

Hata hivyo, vyombo hivyo havikueleza chochote kuhusu mazungumzo ya faragha ya viongozi hao.

“Ngoja nikwambie kitu ndugu yangu. Taarifa inayotolewa kwa waandishi baada ya mazungumzo ni sehemu tu ya kile kilichozungumzwa.

“Kwa mfano, iwapo kuna pande zinapingana, taarifa ya maafikiano itakayotolewa kwa waandishi huwa haielezi kuhusu migongano au ugomvi uliotokea katika mchakato mzima wa kutafuta amani. Kwa hiyo, waandishi huwa mnapewa vitu vidogo sana,” mtoa habari wa gazeti hili ameeleza.

Inadaiwa kuwa rais Kikwete alikutana mara kadhaa na Frazer jijini Addis Ababa, Ethiopia ambapo walijadili mambo mbalimbali ya uongozi nchini na Afrika kwa jumla.

Kwa mujibu wa nafasi yake, Frazer alikuwa na kazi ya kushughulikia masuala ya Afrika na alikuwa akipeleka makao ya wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, taarifa zote za mazungumzo yake na viongozi wa Afrika.

Kikwete anachukuliwa kuwa kiongozi kipenzi cha Marekani katika ukanda wa Mashariki mwa Afrika na Eneo la Maziwa Makuu; nafasi aliyopata akiwa mwenyekiti wa AU, miaka mitatu iliyopita.

Uhusiano huo wa karibu na utawala wa Marekani ulizua utata Septemba 2006, wakati habari zilipovuja kuwa akiwa jijini Washington, rais alikutana na aliyekuwa Rais wa Marekani, George W. Bush na kuongelea hali tete ya kisiasa Kenya.

Hakuna taarifa iliyowahi kutolewa kuhusu walichozungumza, ingawa kuna uwezekano mazungumzo hayo yalirekodiwa na kuna hofu ya kuwekwa wazi na mtandao wa WikiLeaks.

0
No votes yet
Soma zaidi kuhusu:
ingine kilichojionyesha katika mkutano wa Bagamoyo, ni siasa za makundi kuhamia ndani ya kanisa hili kubwa nchini. cheap advertising|made in china

KIKWETE NI KIONGOZI DHAIFU!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kweli dhaifu haswaaaaa!!!!!!!!!!
shedrack

watu waliomchagua mwaka 2005 niliwaambia mapema sana ila hawakunielewa,kuwajaza matozi ikulutu,kiongozi dhaifu,asiyethubutu kukemea mabaya,hana hoja,kazi kujipendekeza kwa wazungu,HUYU MTU NI HEWA JAMANI.

SERIKALI inayoongozwa na Chama cha mapinduzi na sawa na POPO wanata kuinyea mbingu na Wamelala vichwa chini miguu juu hivyo kila muda wanajichafua,one day tutawabandua huo uchafu nyuma yao.

jamani wananchi tujenge hoja ushabiki umeifikisha nchi hii pabaya sana, katiba mpya ndio suluhisho kwa matatizo ya nchi yetu, hakika nawambia ni mpumbavu tu ndio hufanya mambo yale yale kila siku, na hakuna kitu kibaya kama jambo baya linafanyika halafu watu wanakaa kimya na ni jambo baya sana kitu kibaya kinafanyika halafu watu wanaelewa kwamba ni kibaya lakini wanakaa kimya ati kwa ajili tu ya ushabiki. nashukuru kuwa watanzania wengi sasa tumeamka tumechoka na kofia, shati na vitege vya msimu.
tunaitaka mbingu lakini tunaogopa kufa

katika huu uwanja wa maoni.maoni nilazima ya tofautiane.nakubaliana na wale wote wanao ona umuhimu wa nguvu ya hoja.matusi na kukebehiana sio msingi mzuri wa mijadala yenye afya. katiba ni mjadala mzito kwetu sisi sote wa tanzania kulijadili bila ya ushabiki.tukosoane,tutofautiane,lakini bila chuki, bila ugomvi,bila kutukanana. nusu karne baada ya kupata uhuru toka kwa wakoloni,si jambo la kushangaza wananchi kuona haja ya kuwa na katiba mpya.ili kuondokana na ukiritimba wa katiba ya sasa. cha msingi kwa wale ambao wame isoma katiba ya sasa. ni vema basi tuyaseme maeneo yale ambayo yana utata,ili yarekebishwe katika katiba mpya.kf mawaziri kuteuliwa kutokana na wabunge walio chaguliwa na wananchi katika majimbo. je wana watumikia ipasavyo wapiga kura wao? au inapopaswa kutoa uamuzi wa kupeleka barabara ya lami eneo fulani la nchi.je waziri mwenye dhamana hiyo hata pindisha na kupeleka mkoa/eneo anakotoka."conflict of intrest".kwa kifupi mijadala yetu humu ilenge kuelimishana juu ya mapungufu ya katiba ya sasa.ili hiyo katiba mpya tunayo ililia iweze kukudhi haja na matarajio ya watanzania wote.na mwisho mhariri tafadhali fanya kazi yako ya "moderator".Au sio kila mtoa maoni mwenye mihemko atamalizia mihemko yake hapa.

uzee dawa,ujana tiba.

katika huu uwanja wa maoni.maoni nilazima ya tofautiane.nakubaliana na wale wote wanao ona umuhimu wa nguvu ya hoja.matusi na kukebehiana sio msingi mzuri wa mijadala yenye afya. katiba ni mjadala mzito kwetu sisi sote wa tanzania kulijadili bila ya ushabiki.tukosoane,tutofautiane,lakini bila chuki, bila ugomvi,bila kutukanana. nusu karne baada ya kupata uhuru toka kwa wakoloni,si jambo la kushangaza wananchi kuona haja ya kuwa na katiba mpya.ili kuondokana na ukiritimba wa katiba ya sasa. cha msingi kwa wale ambao wame isoma katiba ya sasa. ni vema basi tuyaseme maeneo yale ambayo yana utata,ili yarekebishwe katika katiba mpya.kf mawaziri kuteuliwa kutokana na wabunge walio chaguliwa na wananchi katika majimbo. je wana watumikia ipasavyo wapiga kura wao? au inapopaswa kutoa uamuzi wa kupeleka barabara ya lami eneo fulani la nchi.je waziri mwenye dhamana hiyo hata pindisha na kupeleka mkoa/eneo anakotoka."conflict of intrest".kwa kifupi mijadala yetu humu ilenge kuelimishana juu ya mapungufu ya katiba ya sasa.ili hiyo katiba mpya tunayo ililia iweze kukudhi haja na matarajio ya watanzania wote.na mwisho mhariri tafadhali fanya kazi yako ya "moderator".Au sio kila mtoa maoni mwenye mihemko atamalizia mihemko yake hapa.

katika maisha haya na miongoni mw mambo mengi yanayotokea ninaweza kusema kuwa nawapongeza sana gazeti hili la Mwanahalisi wa kutuletea habari zuri zenye kutufumbua macho. Amani ya Tanzania itakwisha ikiwa chini ya Kikwete,.Nawaomba washauri wa kikwete kabla ya kfanya jambo au baada lazima wafanye utambuzi.
NAMKUMBUKA SANA MwlJulius Nyerer Alihutubia Iringa mwaka 1995 Alisema kuwa Zanzibar ikijitenga ikisema kuwa sisi wazanzibari wao tanganyika sababu ya ulevi tu mambo yote ya ndani hayata kuwa siri tena.

ona sasa tunaelekea wapi? Amani ya Tanzania imepotea Wananchi ya nchi yao wanauwawa na polisi tena kwa risasi nini maana yake? Au ni kwa sababu ya hawafanyi mazoezi ya vita?

tanzania tusipo angalia vita ya kisiasa itatokea.Angalia wenzetu Ivory Coast.

Nakuomba Kikwete tumia busara Wewe si kiongozi bora ila ni MTAWALA.

Hivi sakata la umeme wa Tannzania hatuna wataalamu walio somea mambo ya umeme walio maofisini wanangojea kupata mishahara wasioifanyia kaza? Kama awawezi kubuni mbinu za kutatua tatizo la umeme basi waachi ngazi serikali ikodi wataalamu kutoka nje, au watembelee nchi jirani waone wanavyopata umeme.
Na KRIS BANDIO KARAGWE

Tusiwahumu ambao hawajaridhuka na maneno ya Rais Kwa sababu hatujui wamefikia nini, lakini mimi naweza kusema kuwa wako sahihi kutokana na jinsi mambo yanavyoenda. Mwanasheria Mkuu wa serikari alipinga katiba mpya sasa jiulize alitoa wapi huo uamuzi kama sio kwa amri jeshi mkuu, kama wewe ni mchunguzi utagundua kuwa Rais anaongea maneno mazuri kwa wananchi, lakini ukiangalia upande wa pili viongozi wengine wako tofauti kabisa kwa hiyo inamaana wako kinyume na Rais wakati ni uongozi mmoja. Nafikiri umepata kwann watu wanahoji alichokisema rais inawezekana amesema hivyo to ili kupunguza makali na sio nia njema.

JK ni mwongo wa kutupwa na anawapaka wenzake mafuta kwa mgongo wa chupa kisha anajisafisha kwa wananchi ili aonekane yeye ndio anafaa na sio wataalamu.Hii ni mbaya kwa raisi na taifa kwani raisi hatakiwi kusema lolote kabla ya kushauriana na wataalamu. kwa mfano kwa masuala ya katiba kombani na mwanasheria mkuu werwma ndio washauri wake lakini anakuwa tofauti nao. Sidhani kama yupo tayari kwa ushauri la sivyo wasingejichanganya

kwa suala la umeme namnukuu;
"Nawapongeza viongozi wa Tanesco kwa uamuzi wao wa busara wa kuachana na nia yao ya kununua mitambo ya Dowans. Wameyasoma vizuri mazingira na nyakati na kufanya uamuzi mwafaka.

"Tutahakikisha nchi haiwi gizani na kwamba umeme wa ziada unaotakiwa utapatikana na shughuli za uzalishaji mali na utoaji huduma zitaendelea kama kawaida"" je nchi kwa sasa haipo gizani?????

na wakati huo huo mtaalamu wake alisema ukweli na kukemewa.
mgao huu hauna uhusiano na ile hadhari aliyoitoa Dk. Idris Rashid, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, alipokuwa akizungumzia suala la Dowans kuwa nchi inaweza kuingia kwenye giza siku za usoni," alisema. je nchi haipo gizani?????
na je kwa nn tunalipa dowans pesa sawa na zile au chini kidogo na zile za kununua mitambo yake?????
hapa tuna viongozi kweli wenye kufikiria???? na je wana mpango wa kujenga nchi au kubomoa?
sasa imefika wakati wa wanasiasa kuchukua na kufanyia kazi ushauri wa wataalamu na kuacha woga kwamba watapoteza uwezo wao wa ushawishi wa jamiiii
mungu ibariki tanzania na utuondoshe na hawa viongozi wasiyo na haya kuhujumu nchi.

JAMANi KAMA rais mwenyewe amekubari katiba mpya marumbano ya nini
kilichokuwa kinasubiliwa si kimeshaanza . Jaman Watanzania tuwe wamoja haya yataisha tusianze kufikili mambo mengine kabla ya kusikia maendeleo yako je?

tulichokitaka tumekipata bt isiwe danganya TOTO mchakato uwe wa uhuru maana wapo wanaotaka katiba iwe na manufaa ktk tabaka lao.

p.charles

wapenzi na wasomaji wa MWANAhalisi najua wasomaji wa gazeti hili niwale wapendao mabadiliko na wasiopenda ufisadi na uozo wote wa CCM. Sasa hawa wanaotwambia hatuna hoja tunabwata kuhusu katiba mpya nikwasababu baba zao na ndugu zao wanawanufaisha kupitia hii KATIBA VIRAKA kwakuwapa zabuni fisadi kama za RICHIMOND. Sasa kwataarifa yenu enyi watoto wa mafisadi hatukai kimya tutapiga kelele mpaka kwa baba fisadi JK. Hamuwezi kuzuia nguvu ya uma ,PEOPLES POWER

we vipi???? kwani kila msomaji wa gazeti hili anapenda mabadiliko yasiyo na faida kwa taifa?? wengine humu tunasoma upuuzi wenu, mmeshindwa kunya mtori huko kaskazini mnakuja hapa mjini kutupa tabu tu, ni nani anyeweza kuleta mabadiliko katika nchi hii zaidi ya ccm? we rudi huko kaskazini ukanywe mtori na kufuga nguruwe manake ndo kazi mnayoiweza sio kuongoza nchi, na tunavyowajua wachaga tukiwapa nchi hii wataimaliza kwa kugawana mali zote za nchii kwa dakika tano. hatuwapi nchi hata siku moja. hamna lolote kutwa nzima ni maneno yasiyo na kichwa wala miguu, mnabwabwaja tu bila mpango. we vipi??????

mimi nimefurahi na kauli ya raisi ya mchakato wa katiba mpya. sasa kilichobaki ni watanzania kuacha tofauti zote na kutoa mawazo endelevu ya namna ya kupata katiba mpya. kwa pamoja na umoja kila jambo jema linawezekana. Mungu ibariki afrika na mungu ibariki Tanzania.

CHADEMA Oyeeeeeeeee........ Watanzania kaeni mkao wa Kula.... Tatizo sahani ni moja lakini walaji ni wengi. Mjadala wa Katiba ni sawa na watu milioni 45 kula chakula kwnye sahani moja. Lazima kila mmoja awe chonjo hapo. Hakuna kulala, tusipokuwa makini na utaratibu huu wa Rais wa kuunda Tume, huenda tukarudi kulekule, viraka, kisha Welema akatukebehi huko mbeleni... Lazima kila mtanzania asikurupuke kweli, kuna watu hawajui nini kibaya kwenye Katiba yetu, jamani, kweli hasa wa mjini??? Itafuteni muone ilivyo hoi!!! Tunanyimwa haki sisi raia, ndo maana hata juzi kaamua mwenyewe kuhusu Katiba. Ulishaona Chama au Shirika au Taasisi ya watu yenye Katiba inaamriwa na Mwenyekiti kwamba tubadili Katiba bila kutumia Mkutano Mkuu?? Nchi ni Taasisi, wabunge ambao wawakilishi wetu walitakiwa kupewa kazi hiyo, tume ikaundwa nao na wakaja na mapendekezo ya namna Katiba Mpya inatakiwa kuwa. Hatma ya njanja hii itakuwa kama Tume za akina Jaji Nyarari na Kisanga.

wacha kubwabwaja kama chiriku.Mawazo ya katiba mpya yawakilishwe na makundi ya aina zote na si wanasiasa,wengi wa wanasiasa wapo kwa maslahi yao na mabwana zao,wapo tayari kushawishi watu kumwaga damu kwa maslahi yao,i hate them all!!

Kikwete asiunde Kamati ya katiba! Kazi ya kuunda tume ya katiba iwe ya Bunge na sio ya Kikwete. Suala la mabadiliko ya katiba haliko katika ilani ya uchaguzi ya CCM. Hivi basi Kikwete ajiondoe katika kuteua tume. Nina wasiwasi hiyo tume haitakuwa tofauti na tume ya uchaguzi ambayo ni ya CCM. Wateule wa rais watawajibika kwa rais, lakini wateule wa bunge watawajibika bungeni, bunge ambalo ni la wananchi wenyewe.

Watanzania kuweni macho, ndio kwanza uchakachuaji mwingine wa katiba unaanza. Kikwete asiingilie mchakato wa katiba kwa masilahi binafsi ya kulindana. Hiyo tume itaundwa na akina nani? Kinana, Makamba na Lowasa? Kikwete acha bunge la wananchi liwe huru kuendesha mchakato wa katiba mpya. Acha bunge liwe na uhuru kamili wa kuteua watu wa kada mbalimbali.

wapenzi na wanachama cha CHADEMA mapambano yaendelee kama yalivoanza. Katiba ndo hiyo inakuja kwani kiongozi wa chama cha wachakachuaji ameshapuliza kipyenga cha mchakato. Hawa kina AG Werema na Kombani hawajui hata nini kinaendelea ndani ya Serikali wanayoitumikia,wapo kwaajili yakupokea posho za vikao fake na mishahara ya kodi zetu tu. Peoples power mpaka kieleweke

mpaka kieleweke! ndo msemo gani huo kama si uchakachuaji wa amani???
mwenye busara ameshatangaza kuanza mchakato wa katiba mpya mnayoitaka kuingilia ikulu, sasa subirini hiyo katiba ije sio mnakaa kuropoka kiushabiki eti mpaka kieleweke, kuwa mstaarabu katika maneno yako, usidhani kikwete kukubali kuandikwa katiba mpya ni hasara kwa nchi au serikali au ccm, ni faida kwa wote wala hamuwezi kunishinikiza mnayoyataka nyie wababaishaji, tena kaa kimya pumbavu mkubwa we usiye na haya.

Wewe ni shabiki tu jenga hoja, sioni ulicho comment zaidi ya kujawa ghadhabu za ushabiki,
kaka welcome to the new era

PALE ULIPOANZA KUWEKA MAWAZO YAKO NILIDHANI NI MTU MWENYE BUSARA ZAKE NA PENGINE UNGELIKUWA NA LUGHA TOFAUTI NA VIJANA KUMBE HUNA LOLOTE UNALOLIELEWA. UMEONYESHA WAZI ULIVYO NA UFAHAMU TATA KAMA WA WAJOMBA ZAKO WANAOPIGA POROJO NA KUTOA KAULI ZINAZOPINGANA NA MSIMAMO WA MKUU WA NCHI. WAO WANASEMA HAKUNA KATIBA MPYA MKUU ANASEMA ATAUNDA JOPO. KUWENI WAANGALIFU MSIJE MKAONEKANA MNA UFAHAMU MDOGO WA KUYAJUA MAMBO. SOMENI NYAKATI.

Nimeshangazwa na kauli ya msomaji,aliyeandika hapo juu,baada ya yule mwanzo kutoa maoni yake,sitaki mambo ya Burundi,Rwanda na kwingineko ambako mwandishi hapo juu inawezekana anatoka huko.Watanzania hatujafikia kutukanana,aliyeandika hapo juu yawezekana si raia wa nchi hii.Anaonekana ni mgomvi,kama kuna tatizo jenga hoja.Tanzania ni nchi yetu sote tunahitaji kupendana.Mungu ibariki Tanzania.wachovu wa mawazo ,wanaotukana wenzao kama mwenzangu hapo juu wanyong'onyee nawashindwe.Mwandishi ukiona ujumbewakutukanana usiuchapishe tafadhari

wewe naye ndo walewale! umebaki kuangalia upande mmoja tu! sasa hapa nani katukana? je hao wanawaita viongozi wa nchi (raisi) kuwa hafai kuongoza hata mke wake na watoto hayo si matusi? eti waziri ngeleja ni msukuma mshamba hafai kuwa hata balozi wa nyumba 10, mara raisi ni mwizi mnafiki, muongo na mesngine mengi tu, sasa huo ndo ustaarabu? au huko ndo kujenga hoja? sioni hata kama kuna kujenga hoja humu gazetini, wote wamebaki kuwadhalilisha viongozi mbele ya raia zao na familia zao, unapomuita mtu ni mwizi au muongo au mnafiki wakati huna uhakika na ukisemacho huoni kama wewe ndo muongo na mzushi?
kuweni wastaarabu nyie kwanza ndo wengine wawe wastaarabu, (nyani haoni kundule) mnatukana kutwa nzima humu gazetini halafu mnasema tujenge hoja ni hoja gani hiyo mnayoijenga humu? kudhalilisha watu ndo kujenga hoja???????? kaa pembeni usifatilie watu.

JAMANI UMESIKIA RAISI ALIVYOSEMA KUHUSU KATIBA?

Sasa Jaji Werema wakati anatoa maoni yake kuhusu katiba alikuwa ame base wapi? au alikuwa hajui ofisi yake imemshauri nini Rais? au Ikulu imeamua nini kuhusu ushauri alioutoa? Sielewi vizuri haya mambo yanavyokwenda

Celina Kombani -- Serikali haina pesa wala bajeti ya kuandaa katiba mpya

PM Pinda: Serikali inalipokea swala la katiba mpya, italifanyia kazi kwa kumshauri Rais

AG Werema: Katiba mpya hapana, tuweke viraka kwenye hii iliyopo kama ni lazima

President: Anakubali katiba mpya ni muhimu, na ataunda tume kushughulikia hilo

Haya yote ni ndani ya siku 60 baada ya uchaguzi.
KWA KWELI SERIKALI YA CCM NI USANII MTUPU............CHADEMA TUKOMAE MPAKA KIELEWEKE

sasa nyie ni wagomvi tena ni maharamia! rais ametangaza kuanza mchakato wa katiba mpya halafu unasema hamkubali mpaka kieleweke!!!!!!!!!!!! mnataka nini zaidi ya hapo kama si ugomvi? punda we usiyeitakia mema nchi hii.

Tafadhali tumia lugha nyepesi mwana CCM,maana najua hukufurahia hili!

tena hawa jamaa chama cha wachaga ni wajinga kabisa,sasa ni zamu yao kupokea matusi