HABARI MAHUSUSI

Chenge kufuru tupu, amiliki bilioni 25

Na Saed Kubenea 15 Apr 2008

Amchotea kigogo bilioni moja
Amwashia indiketa Ben Mkapa

WAZIRI wa Miundombinu, Andrew Chenge anaogelea katika utajiri wa zaidi ya Sh. 25 bilioni zenye utata huku Rais Jakaya Kikwete akiendelea kumkumbatia, MwanaHALISI limegundua.

 
Na Mwandishi Wetu 15 Apr 2008

MBUNGE wa Igunga (CCM), Rostam Aziz, ametishia kujiuzulu ubunge kutokana na hatua ya Kamati ya Uongozi ya Bunge kumzuia kuwasilisha hoja yake bungeni, MwanaHALISI limedokezwa.

 
Na Mwandishi Maalum 15 Apr 2008

SERIKALI imepandikiza chuki. Wiki iliyopita, ilitangaza kulipia mishahara ya wafanyakazi wa Kampuni ya Reli (TRL), ambao walishindwa kulipwa na muwekezaji aliyekodishwa shirika hilo.

 
Na Mbasha Asenga 15 Apr 2008

YAPO mambo mengi aliyozushiwa Andrew Chenge, Waziri wa Miundombinu ambayo mengi watu waliyaona kama mambo ya mtaani tu. Kwa mfano, niliwahi kusikia Chenge alikuwa akisafirisha suti zake kwa DHL kwenda London, Uingereza kufuliwa.

 

MUAFAKA uliotarajiwa kuwa mwanzo wa hatua muhimu za kuleta ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro wa kisiasa Zanzibar, umekwama.

11/04/2010